Wednesday, July 27, 2016

SERIKALI YAILIPA BHARTI AITEL BILIONI 14.9, TTCL SASA KAZI TU

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Profesa Makame Mnyaa Mbarawa (kulia) akizungumza kwenye mkutano wake na Wafanyakazi wa Kampuni ya TTCL wa Makao Makuu na Ofisi za Mkoa wa Dar Es Salaam ulofanyika leo katika Ukumbi wa Water Front jijini Dar es Salaam.
 
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Profesa Makame Mnyaa Mbarawa akizungumza kwenye mkutano wake na Wafanyakazi wa Kampuni ya TTCL wa Makao Makuu na Ofisi za Mkoa wa Dar Es Salaam ulofanyika leo katika Ukumbi wa Water Front jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL, Profesa Tolly Mbwete (kulia) akizungumza kwenye mkutano wa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Profesa Makame Mnyaa Mbarawa pamoja na Wafanyakazi wa Kampuni ya TTCL wa Makao Makuu na Ofisi za Mkoa wa Dar Es Salaam leo katika Ukumbi wa Water Front jijini Dar es Salaam. Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Dk. Kamugisha Kazaura (kulia aliyesimama) akizungumza kwenye mkutano wa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Profesa Makame Mnyaa Mbarawa pamoja na Wafanyakazi wa Kampuni ya TTCL wa Makao Makuu na Ofisi za Mkoa wa Dar Es Salaam leo katika Ukumbi wa Water Front jijini Dar es Salaam. Baadhi ya Wafanyakazi wa Kampuni ya TTCL wa Makao Makuu na Ofisi za Mkoa wa Dar Es Salaam wakiwa katika mkutano wao na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Profesa Makame Mnyaa Mbarawa ulofanyika leo katika Ukumbi wa Water Front jijini Dar es Salaam. Baadhi ya Wafanyakazi wa Kampuni ya TTCL wa Makao Makuu na Ofisi za Mkoa wa Dar Es Salaam wakiwa katika mkutano wao na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Profesa Makame Mnyaa Mbarawa ulofanyika leo katika Ukumbi wa Water Front jijini Dar es Salaam. Baadhi ya Wafanyakazi wa Kampuni ya TTCL wa Makao Makuu na Ofisi za Mkoa wa Dar Es Salaam wakiwa katika mkutano wao na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Profesa Makame Mnyaa Mbarawa ulofanyika leo katika Ukumbi wa Water Front jijini Dar es Salaam. Sehemu ya Wafanyakazi wa Kampuni ya TTCL wa Makao Makuu na Ofisi za Mkoa wa Dar Es Salaam wakiwa katika mkutano wao na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Profesa Makame Mnyaa Mbarawa ulofanyika leo katika Ukumbi wa Water Front jijini Dar es Salaam. Sehemu ya Wafanyakazi wa Kampuni ya TTCL wa Makao Makuu na Ofisi za Mkoa wa Dar Es Salaam wakiwa katika mkutano wao na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Profesa Makame Mnyaa Mbarawa ulofanyika leo katika Ukumbi wa Water Front jijini Dar es Salaam. Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Profesa Makame Mnyaa Mbarawa (kulia) akizungumza kwenye mkutano wake na Wafanyakazi wa Kampuni ya TTCL wa Makao Makuu na Ofisi za Mkoa wa Dar Es Salaam ulofanyika leo katika Ukumbi wa Water Front jijini Dar es Salaam. Baadhi ya maofisa wa Kampuni ya TTCL wa Makao Makuu na Ofisi za Mkoa wa Dar Es Salaam pamoja na maofisa kutoka wizara ya Ujezi, Uchukuzi na Mawasiliano wakiwa katika mkutano wao na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Profesa Makame Mnyaa Mbarawa ulofanyika leo katika Ukumbi wa Water Front jijini Dar es Salaam. Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Profesa Makame Mnyaa Mbarawa (kushoto) akishirikishwa jambo na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Dk. Kamugisha Kazaura (kulia) katika ofisi za Kampuni ya TTCL Makao makuu kabla ya kuzungumza na wafanyakazi.

WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe Profesa Makame Mnyaa Mbarawa amesema, Serikali imemalizana kimalipo na kampuni mbia wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) hivyo anataka kuiona TTCL ikizaliwa upya na kutoa ushindani wa hali ya juu katika soko la Mawasiliano nchini. 

Waziri Mbarawa ameyasema hayo Jijini Dar Es Salaam leo alipokuwa akizungumza na Wafanyakazi wa Kampuni ya TTCL wa Makao Makuu na Ofisi za Mkoa wa Dar Es Salaam. Akizungumza katika mkutano huo alisema serikali imefanya mengi katika kuiwezesha TTCL kuwepo na kuendelea kuhudumia Watanzania.

 "...Siku chache zilizopita, tumeilipa Bharti Airtel shilingi bilioni 14.9 na kuachana rasmi na kampuni hiyo," alisema Waziri Prof. Mbarawa. "Ndugu Wafanyakazi, sasa ni wakati wa kufanya kazi. 

Hatuna tena muda wa kupoteza, muda tulionao ni wa kuwajibika, kuwatumikia Wananchi. Serikali inafanya kila jitihada kuwawezesha. Tunachotaka kwenu ni uadilifu, hatuna nafasi kwa wabadhirifu, wavivu na wanaovujisha siri za kampuni kwa washindani. 

Ni lazima mbadilike na mfanye kazi kwa juhudi kubwa sana, Wananchi waridhike," alisisitiza Prof. Mbarawa. Awali akitoa taarifa fupi kwa Waziri, Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Dk. Kamugisha Kazaura alisema, kampuni hiyo inashukuru mchango mkubwa wa Serikali katika kuiwezesha ili kuendelea kutimiza vyema wajibu wake. 

"...Mhe Waziri, tunaishukuru sana Serikali na wewe binafsi kwa jitihada kubwa ambazo zimetufikisha hapa tulipo," alisema Dk. Kazaura katika taarifa yake. Akitaja baadhi ya jitihada za Serikali, alisema imefanikisha kuiondosha Kampuni ya Bharti Airtel ndani ya TTCL, kuisamehe TTCL madeni ya takribani shilingi bilioni 100, Serikali kuipatia TTCL masafa ya Mawasiliano na kibali cha kutumia rasilimali zake kama dhamana ili kupata fedha za kufanikisha mipango na mikakati yake ya kibiashara. 

Aidha Dk. Kazaura alisema, kutokana na mchango huu mkubwa wa Serikali, Kampuni hiyo imeongeza kwa kiasi kikubwa ufanisi wake ikiwa ni pamoja na kuanzishwa kwa huduma za 4G LTE ambazo hadi sasa zimesambaa katika maeneo 33 Jijini Dar Es Salaam huku mpango ukiwa ni kufikisha huduma hizo Jiji zima la Dar es salaam na mikoa mingine mitatu ifikapo mapema mwakani.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL, Profesa Tolly Mbwete akizungumza katika mkutano huo alisema kampuni hiyo imejipanga kikamilifu katika kutoa huduma bora na za kiwango cha juu kabisa katika huduma za Mawasiliano nchini ikiwa ni pamoja na kukabiliana na changamoto zilizopo katika sekta hiyo kwa weledi na ububifu wa hali ya juu.

No comments: