Thursday, July 14, 2016

MBUNGE WA MKURANGA ULEGA AKABIDHI MADAWATI 100 KWA SHULE YA MSINGI KIPALA KATIKA KATA YA MWANDEGE.

Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega akizungumza na wananchi wa Mwandege wakati hafla ya kukabidhi madawati 100 kwa shule ya msingi Kipala katika kijiji cha Mwandege Wilaya Mkuranga mkoani Pwani leo.
Diwani wa Kata ya Mwandege, Adoph Kowero akitoa akizungumza na wananchi wa mwandege katika hafla ya kupokea madawati 100 yalitolewa na Mbunge wa Mkuranga ,Abdallah Ulega katika hafla iliyofanyika katika viwanja vya shule ya msingi kipala leo.
Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule ya Msingi Kipala, Halima Dikeche akisoma risala kwa mbunge wa jimbo la Mkuranga, Abdallah Ulega  juu ya changamoto ya madawati katika hafla ya mbunge wa jimbo hilo kukabidhi madawati 100 kwa shule hiyo.
Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega akikabidhi moja ya dawati Mwalimu  Mkuu shule ya Kipala,Ramadhan Haji katika hafla iliyofanyika katika viwanja vya shule ya msingi kipala leo.
Sehemu ya wanafunzi wakiwa wamekaa katika madawati mapya yalikabidhiwa na mbunge wa jimbo la Mkuranga leo katika hafla iliyofanyika katika viwanja vya shule ya msingi kipala.
Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega akizungumza na wananchi leo Mkuranga.
Sehemu ya Wananchi wakimsikiliza Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega katika hafla  ya kukabidhi madawati  100 iliyofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Kipala leo.
 (Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii)

No comments: