Wednesday, July 6, 2016

HALMASHAURI ZA UVINZA NA BUHIGWE ZAPEWA MAFUNZO YA UTEKELEZAJI WA MRADI WA PS3 MKOANI KIGOMA

Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe mkoani Kihoma, Kanali Marco Gaguti akizungumza leo wakati wa mafunzo ya siku moja kwa watendaji wa halamshauri mbili za Buhigwe na Uvinza ambazo zimechaguliwa kuanza utekelezaji wa awamu ya kwanza ya mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya sekta za Umma (PS3) unaofadhiliwa na Serikali ya Marekani kupitia Shirika lake la Misaada la Kimataifa (USAID).
Kanali Gaguti aliwataka watumishi hao wa halmashauri hizo mbili kuchukulia fursa hiyo ya kuanza utekelezaji wa ,radi huo kwa umuhimu kubwa kwani kuanza kwao ni kutokana na changamoto zilizipo katika Halmashauri zao.

"Tutumie fursa hii kikamilifu ili kukabiliana na changamoto zilizopo katika halmashauri zetu, tumeona kuwa tuna miradi mingi katika maeneo yetu lakini hatuitumii vizuri kutusaidia hivyo tuanze mradi huu wa PS3 kwa kumbukumbu kwa kupiga hatua nzuri ili tuondoke hapa tulipo katika changamoto,"alisema Kanali Gaguti.
 Washiriki wa kutoka Halmashauri za Uvinza na Buhigwe wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe.
Mwanasheria wa Kigoma Grace Letawo akifuatilia mijada
 Mijada katika makundi ilianza kwa ajili ya utambuzi wa wadau mbalimbali wa maendeleo katika Halmashauri. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.
 Mshauri wa Masuala ya Utawala Bora wa Mradi wa PS3, Joel Shimba akifafanua jambo alipokuwa na kundi la Halmashauri ya Uvinza.
 Washiriki kutoka Halamashauri ya Wilaya ya Buhigwe, wakiwa katika mjadala wa kundi lao.
 Mtaalam wa masuala ya uongozi kutoka Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo (LGTI) akifafanua jambo.
 Mshauri wa Masuala ya Utawala bora wa mradi wa PS3, Nazar Sola akifuatilia kwa makini mjadala katika moja ya makundi.
 Mkurugenzi wa shughuli za mikoa wa PS3, Dk Conrad Mbuya akifuatilia kwa makini mijadala katika makundi ambayo yalikuwa yakifanya utambuzi wa wadau wengine katika Halmashauri na kuangalia namna ambavyo shughuli za wadau zilikuwa zikiratibiwa. Pia makundi yalipaswa kuangalia maeneo ambayo mradi unaweza kushirikiana na sekta binafsi ili kuimarisha mifumo ya sekta za umma.
 Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe, Kanali Marko Gaguti akifuatilia kwa makini mjadala katika Halamashauri yake.
 Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza, Benard Rusomyo akiwasilisha taarifa ya Wilaya yake.
Mwakilishi wa Halamashauri ya Buhigwe, ambaye ni Afisa Elimu ya Msingi, Mwl. Freddy Fande akiwasilisha taarifa ya Halmashauri hiyo.
 
 Mshauri wa Masuala ya Fedha wa PS3, Victor Msoma akizungumza jambo baada ya mawasilisho ya Halmashauri.

No comments: