Tuesday, June 28, 2016

wengine 10 waibuka milionea droo ya 5 ya tusker fanya kweli Na uwini.


Afisa Mkaguzi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini Juhudi Ngolo(kushoto) akihakiki taarifa za moja ya mshindi kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Masoko kwa Wateja kutoka Kampuni ya Bia ya Serengeti Lulu John Mduma(kulia)
Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Masoko kwa Wateja kutoka Kampuni ya Bia ya Serengeti Lulu John Mduma akiongea kwa njia ya simu na mmoja wa washindi wa droo ya tano ya Tusker Fanya Kweli Uwini
Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Masoko kwa Wateja kutoka Kampuni ya Bia ya Serengeti Lulu John Mduma akitoa ufanunuzi zaid wakati wa droo ya tano ya Milioni 100 na Tusker Fanya Kweli Uwini
Meneja Rasilimali Watu wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Paul Hamidu Kimasharo(kushoto) akichezesha droo ya tano ya Tusker Fanya Kweli Uwini huku akishuhudiwa na Afisa Mkaguzi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini Juhudi Ngolo(wa pili kushoto) pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Masoko kwa Wateja kutoka Kampuni ya Bia ya Serengeti Lulu John Mduma(wa pili kulia) na mtangazaji wa ITV Abdallah Mwaipaya(kulia).

Promosheni ya aina yake inaendelea huku watanzania wengi zaidi wakibadilisha maisha yao.
27 Juni, 2016: Baada ya kutoa washindi ishirini kwa mara moja wiki iliyopita jana kupitia promosheni inayoendeshwa na Kampuni ya Bia ya Serengeti ijulikanayo kama Tusker Fanya Kweli Uwini imeendelea huku washindi wengine kumi wakipatikana katika droo ya tano ya promosheni hiyo kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini. Washindi hao wanafanya jumla ya idadi yote kufikia washindi sitini mpaka sasa waliojipatia Milioni moja kila mmoja. 
 
Katika kampeni hii inayoendelea ya Tusker Fanya Kweli Uwini tayari washindi 50 walikabidhiwa fedha zao katika hafla za makabidhiano zinazofanyika kila wiki. Washindi wote ambao tayari wameshapokea pesa hizo wameshuhudia kupokea pesa zao kwa utaratibu mzuri. Million 60 tayari zimeshaenda kwa washindi wa promosheni hiyo, bado Milioni 40 kushindaniwa.

Droo hiyo ya 5 iliyofanyika katika studio za ITV jana, ilirushwa kupitia televisheni hiyo, huku ikishuhudiwa na Afisa kutoka bodi ya michezo ya kubahatisha nchini na wadau wengine nao walishuhudia kwa umakini kila droo ilivyofanyika na uhalisia wake. Wafuatao walitangazwa kuwa washindi wa droo ya 5; Fatma Abuu kutoka Morogoro, Hassan Rajabu kutoka Dodoma, Patrick Kimaro na Philiasi John kutoka Mwanza, Bakari Rashidi anayetoka katika mkoa wa Pwani, Lucy J.Mosile pamoja na Deodatus John kutoka Dar es salaam. 
 
Washindi wote waliopatikana walikuwa na shauku ya kueleza jinsi walivyoingia katika mashindano na jinsi watakavyotumia pesa hizo walizopata. Washindi wote walipewa maelekezo ya kufika katika hafla ya makabidhiano na jinsi ya kupata pesa zao tayari kwa kuanza safari ya umilionea.

Akiongea kwa njia ya simu mmoja ya washindi wa droo ya tano ya Tusker Fanya Kweli Uwini Lucy Mosile aliishukuru Kampuni ya Bia ya Serengeti kwa kuwapa fursa hiyo waliyoipata ya kuwa milionea. 
 
“Nashukuru sana kwa kupata fursa hii, nilikua na ndoto ya kufuga kuku na samaki lakini sikua na namna ya kujiwezesha kufanya ivo, lakini leo nashukuru sana mana ntatimiza ndoto yangu ya siku nyingi ya kufanya biashara ya kuku kwa kufuga kuku wa nyama na mayai kutokana na hii Milioni moja niliyoipata kutoka Tusker. Sikutegemea kama ningekua moja ya washindi leo hivyo nawasii na wengine waendelee kujaribu wasikate tama.”

Naye Mkuu wa kitengo cha huduma za masoko kwa wateja wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Lulu J. Mduma, alisisitiza kuwa kushiriki zaidi ya mara moja kunampa mtumiaji nafasi ya kushinda mara nyingi zaidi. Bado kuna mamilioni ya kutosha, watumiaji wa bia ya Tusker waendelee kushiriki mara nyingi wawezavyo waweze kuwa mamilionea.
 
 “Tumeshuhudia washindi walioshinda mara mbili. Kwa jinsi unavyoendelea kuburudika na bia ya Tusker, shiriki katika promosheni hii ya kubadilisha maisha na kuwa millionea. Ni ya uhakika, inatokea na inabadilisha maisha ya wateja wetu” Alisema Bi. Lulu

‘Tusker fanya kweli uwini’ ni kampeni ya kitaifa ambayo ilianza kama wiki sita zilizopita ikilenga mikoa yote nchini, mpaka sasa promosheni hiyo imefanya watanzania kujishindia millioni moja kwa kila mmoja, washindi kumi kwa wiki, isipokua wiki iliyopita katika droo ya nne ambapo washindi 20 walipatikana ikiwa ni kuongeza hamasa zidi kwa wateja wa bia ya Tusker kwani Ilizidisha furaha kwa watumiaji wengi zaidi ukilinganisha na wiki zingine. 

No comments: