Na KhadijaKhamis –Maelezo Zanzibar 8/06/2016.
Waziri
wa Afya Mahmoud Thabit Kombo amelizindua rasmi Baraza la Ushauri la
Afya ya Jamii na Mazingira lenye wajumbe nane kutoka sekta za Serikali
na sekta binafsi .
Akizindua
Baraza hilo katika Wizara ya Afya Mnazimmoja, alisema lengo la kuundwa
Baraza hilo ni kudhibiti hali ya afya na mazingira ili kuisaidia jamii
kujiepusha na maradhi ya mripuko na maradhi ya kuambukiza.
Alisema
Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Muhammed Shein alimteuwa Mwenyekiuti wa
Baraza hilo mwaka 2013 lakini kutoakana na kutokuwepo wajumbe ambao
huteuliwa na Waziri anaehusika na Afya lilishindwa kufanyakazi kwa muda
wote.
Aliwataka
wajumbe hao kuwa wabunifu katika kutafuta fedha za kusaidia kuendesha
kazi bila kutegemea Bajeti ya Wizara kwani fedha wanazopata ni kidogo na
haziwezi kuendesha Baraza kwa ufanisi.Ameeleza matumaini yake kwa
wajumbe hao, kutokana na umahiri wao wa masuala ya Afya na Mazingira,
watafanyakazi kwa mashirikiano na kuleta ufanisi mkubwa kwa jamii ambayo
imetuzunguka .
Nae
Mwenyekiti wa Baraza hilo Omar Juma Khatib alimshukuru Waziri wa Afya
kwa kuona umuhimu wa kuwepo Baraza hilo na kuharakisha kuteuwa wajumbe
kuanza kazi rasmi.Ameahidi kuwa atashirikiana na wajumbe kuhakikisha
kuwa wanapunguza vifo vinavyotokana na mazingira machafu na kutimiza
wajibu wao kwa mujibu wa taratibu na sheria zilizowekwa .
“Wajumbe
kazi iliyopo mbele yetu ni muhimu sana kwani inagusa maisha ya watu
wetu, hivyo tunapaswa kutoa michango na mapendekezo yetu katika
kufanikisha kazi hii, ”alisisitiza Mwenyekiti.Wajumbe wa Baraza hilo
wamemshukuru Waziri kutokana na muda mfupi tokea achukue nafasi hiyo
kuona kunaumuhimu wa kuundwa rasmi Baraza kwa kufanya uteuzi wa wajumbe.
Wameahidi
kuwa watatoa ushirikiano wa karibu kwa Mwenyekiti wao ili kuhakikisha
malengo yaliyowekwa na Serikali ya kuundwa Baraza la Ushauri wa Afya na
Mazingira yanafikiwa .IDARAYA HABARI MAELEZO ZANZIBAR.
Waziri
wa Afya Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo akisoma baadhi ya vifungu vya
sheria ya Baraza la Ushauri la Afya ya Jamii na Mazingira kabla ya
kulizindua Baraza hilo katika hafla iliyofanyika Wizara ya Afya
Zanzibar.
Waziri
wa Afya Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo akimkabidhi sheria Mwenyekiti wa
Baraza la Ushauri la Afya ya Jamii na Mazingira Dk. Omar Juma Khatib
mara baada ya kulizindua.
Mwenyekiti
wa Baraza la Ushauri la Afya ya Jamii na Mazingira Dk. Omar Juma Khatib
akizungumza na wajumbe wa Baraza hilo wakati wa uzinduzi, kushoto yake
Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo.
Mwenyekiti
wa Baraza la Ushauri la Afya ya Jamii na Mazingira Dk. Omar Juma Khatib
akizungumza na wajumbe wa Baraza hilo wakati wa uzinduzi, kushoto yake
Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo.
Waziri
wa Afya Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo akimtakia Kheri Mwenyekiti wa
Baraza la Ushauri la Afya ya Jamii na Mazingira Dk. Omar Juma Khatib
katika utendaji wa kazi zake. Picha na Makame Mshenga/Maelezo Zanzibar.
No comments:
Post a Comment