Saturday, June 4, 2016

WAZIRI MAKAMBA ASHIRIKI KUPANDA MITI YA MIKOKO NA WAKAZI WA KATA YA MBWENI JIJINI DAR LEO

  Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. January Makamba akitia saini kitabu cha Wageni alipotembelea Kata ya Mbweni iliyopo Manispaa ya Kinondoni kwa ajili ya shughuli za upandaji mikoko katika eneo hilo.
    Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. January Makamba akipanda mti aina ya mkoko katika fukwe za bahari ya hindi katika eneo la Mbweni jijini Dar es Salaam. Upandaji huo wa mikoko ni katika kuadhimisha wiki ya mazingira duniani, ambayo kilele chake ni kesho
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. January Makamba  akishirikiana kupanda miti ya mikoko na wakazi wa kata ya  Mbweni jijini Dar es Salaam ikiwa ni kuelekea kilele cha siku ya mazingira hapo tarehe 5 juni.
 . Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. January Makamba akifurahia jambo na Wanafunzi wa Shule ya Msingi Mbweni ambao walijumuika pamoja naye kupanda mikoko katika fukwe za Mbweni jijini Dar es salaam.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. January Makamba akiongea na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) mara baada ya kumaliza kupanda mikoko katika fukwe za bahari ya Hindi katika kata ya Mbweni.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. January Makamba Ametoa wito kwa Wananchi  wa Kata ya Mbweni kutunza mazingira na kutoa kipaumbele kwa mazingira. Aliyasema hayo wakati wa zoez la upandaji mikoko lilifanyika katika fukwe za bahari ya Hindi zilizoko Mbweni.

Akiongoza Wananchi wa Kata hiyo kupanda miche 5,000 ya mikoko , Waziri Mkamba alisititiza pia Wanafunzi wa shule waliopo katika eneo hilo kupenda mazingira yao na kuyatunza ili yawafae baadaye.

Wakisoma Risala yao , Wanawake wa Mbweni walimuomba Waziri awasaidie kuwapatia vitendea kazi  kwa ajili ya kuhudumia mikoko pamoja na kumuomba awasaide kuwatatulia changamoto wanazokutana nazo. Ikiwamo ya maafisa wa TRA kukata hovyo mikoko wanapokua wanafanya doria katika fukwe zaMbweni.

Mwisho Waziri aliwahukuru Wananchi wa Mbweni waliojitypkeza kujumuika naye katika zoezi hilo la upandaji mikoko. Shuhuli za upandaji mikoko ni kuelekea maadhimisho ya siku ya mazingira ambayo kilele chake ni tarehe 5 juni kila mwaka.

No comments: