Monday, June 20, 2016

TUSKER FANYA KWELI UWINI YATOA MILLION 20 KWA WASHINDI 20 WIKI HII

Droo hii ya aina yake yawafanya watanzania 20 kuwa milionea leo! Wateja wa tusker hadi leo wamepokea kiasi cha shilingi za kitanzania Milioni 50 kwenye promosheni inayoendeswa na kampuni ya serengeti kupitia bia ya Tusker iitwayo TUSKER FANYA KWELI NA UWINI. 

Tayari washindi 30 walikwishapatikana na wote wamepata zawadi zao za pesa taslimu. Droo ya leo ambayo ilikuwa ya kusisimua ilikuwa tofauti na droo zingine kwani leo washindi ishirini walitangazwa na sio kumi kama ilivyozoeleka.Promosheni hii imeweza kupata washindi kutoka mikoa mbalimbali na washindi wote wamekubali kwamba maisha yao yamebadilika kwa njia moja au nyingine. 

Wiki iliyopita alipatikana mshindi Bw Albert Tarimo ambaye alionyesha kwa furaha ujenzi wake na kusema kwamba atatumia pesa aliyopata kuweza kuongeza matofali, dhahiri kuwa promosheni hiii imemfanya bw. Albert afanye kweli katika harakati zake za ujenzi. 

Kuna ambao wamekiri kutumia pesa hizi kwa kulipa ada na wengine kuongezea mtaji kwenye biashara zao. Droo za Tusker fanya kweli uwini zinafanyika kila ijumaa katika studio za ITV na kushuhudiwa na afisa wa bodi ya bahati nasibu ya taifa na wadau wengine, huku kipindi hiki kikirushwa itv siku hiyo hiyo ya ijumaa jioni. 

Baadhi ya washindi wa droo hii ya nne ni Grace Richard kutoka Dar Es salaam, Kitula kutoka Kahama shinyanga, Martina Japhet kutoka Tabora, J J Malunga kutoka Shinyanga, kutoka mwanza Mr Isaya Stanley Furaha Mushumbuzi kutoka Morogroro, Ibrahim Faiko kutoka Iringa, Victor Mwingo kutoka Pwani . Washindi wote ishirini walipatikana kwenye simu na walionyesha furaha isiyo na kifani. Walipewa maelekezo jinsi ya kupata hela yao na ili kukamilisha ushindi wao. Washindi wote hukabidhiwa pesa yao katika hafla fupi kila ijumaa huku wakiendelea kuburudika na tusker na burudani kemkem.

Bado kuna zaidi ya million hamsini za kushindaniwa kwa wateja wa tusker. Tangu uzinduzi wa kampeni hii wapenzi wa tusker pamoja na kujishindia pesa taslimu pia wameweza kujipatia zawadi nyingi zikiwemo bia za bure za tusker, tshirt na kofia pamoja na kupata burudani maalum. 

Akiongea kwa furaha, meneja wa Masoko Nandi Mwiyombela amesema kwamba kwa sasa promosheni inaendelea vizuri sana na wameweza kufikia malengo. “Pesa taslimu ina nguvu. Kwa kiingereza wanasema ‘Cash is a strong tool’ na kulingana na yale tunayosikia kutoka kwa washindi wetu tumegundua ya kwamba kwa kweli kuwa na zawadi ya fedha taslimu ilikuwa uamuzi mzuri na kwa uhakika wameelezea kuweka au kutumia pesa zao vizuri. Jambo lililotusukuma mpaka kuamua kupata washindi ishirini na sio kumi kwa leo ni kutokana na hamasa tunayopata kutoka kwa washindi wetu. Washindi wanatokea mikoa mbalimbali, hilo ndilo lengo letu kubwa, kupata washiriki na washindi nchi nzima.”, alisema Bi. Nandi.

“Tusker Fanya Kweli Uwini’ inaendelea, pamoja na washindi ishirini tuliowapata leo mpaka kufikia washindi 50. Tumeshatoa pesa taslimu shilingi milioni 50 na sasa imebaki milioni 50. Pia kama, mnanavyojua promosheni hii pia inawazawadia wahudumu wanaohudumia wateja wetu, hadi kufikia leo tumeweza kuwapatia shilingi milioni 22.” kamalizia Bi. Nandi. 

Mteja wa tusker anaruhusiwa kushiriki mara nyingi awezavyo, amepatikana mteja aliyeibuka mshindi kwa mara ya pili katika hii promosheni ambayo haiendeshwi kwa njia ya kompyuta bali kwa kuchanganya kuponi zilizojazwa na watumiaji wa tusker na kuweza kupata majibu sahihi papo hapo. 
Mkaguzi kutoka Bodi ya michezo ya kubahatisha nchini Madam Chiku (katikati) akihakiki taarifa za washindi 20 wa droo ya nne,kulia kwake ni Joseph Silumbe - Visibility Manager na kushoto kwake ni Meneja wa bia ya Tusker Jasper Migambile.
SBL Visibility Manager Joseph Silumbe (kulia) akichezesha droo ya nne huku akishuhudiwa na mkaguzi kutoka Bodi ya michezo ya kubahatisha nchini Madam Chiku (katikati) pamoja na meneja wa bia ya Tusker Jasper Migambile (kushoto).
SBL Visibility Manager Joseph Silumbe (kulia) akimpa kuponi ya mshindi mkaguzi kutoka bodi ya michezo ya kubahatisha nchini madam Chiku (katikati) huku akishuhudiwa na Meneja wa bia ya Tusker Jasper Migambile (kushoto).

No comments: