Tuesday, June 7, 2016

SSRA YATOA ELIMU YA HIFADHI YA JAMII KWA WAKULIMA, VYUO VYA UALIMU NA VETA KATIKA MIKOA YA RUKWA, KIGOMA NA KATAVI

Mgeni rasmi Kaimu RAS Mkoa wa Rukwa Bw. Abubakary Kunenge, akitoa hotuba wakati wa ufungizi wa semina ya elimu ya Hifadhi ya Jamii kwa wakulima wa MVIWATA Rukwa, Kulia ni Mwenyekiti wa MVIWATA Rukwa Bi. Lydia Ruhilo na kushoto ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Bw. Mohamed Nyasama.
Sehemu ya Wanafunzi wa Chuo cha Ualimu Sumbawanga wakisikiliza kwa makini mada zilizokuwa zikitolewa kutoka SSRA wakati wa Semina ya elimu ya Hifadhi ya Jamii Mkoani Rukwa hivi karibuni.
Afisa wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Bw. Samuel Nzunda akiwasilisha mada wakati wa semina ya elimu ya Hiafadhi ya Jamii mkoani Rukwa.
Wawakilishi kutoka Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), wakiwa katika picha ya pamoja na wakufunzi wa Chuo cha VETA-Kigoma mara baada ya semina ya elimu ya Hifadhi ya Jamii iliyoendeshwa na SSRA mkoani humo hivi karibuni.
Bi Carina Wangwe, kutoka SSRA akifafanua jambo wakati wa semina ya elimu ya Hifadhi ya Jamii kwa wadau mkoani Kigoma.
Afisa kutoka SSRA, Bw. Ally Masaninga akiwasilisha mada wakati wa semina ya elimu ya Hifadhi ya Jamii mkoani Kigoma hivi karibuni.
Wanafunzi wa Chuo cha UfundiStadi – VETA Kigoma wakisikiliza kwa makini mada kutoka kwa maofisa wa SSRA. 
Wawakilishi wa SSRA wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi wa Chuo cha Newma-Kigoma mara baada ya semina ya elimu ya Hifadhi ya Jamii kwa wanafunzi wa Chuo hicho.
Bw. Onorius Njole, Mkurugenzi wa Huduma za Sheria kutoka SSRA akifafanua jambo wakati wa semina kwa wadau wa Chuo cha Ualimu Mpanda.
Wanafunzi wa Chuo cha Ufundi Stadi – VETA Mpanda wakisikiliza kwa makini mada kutoka SSRA.
Afisa kutoka SSRA Bi. Beatrice Ngong’ho akigawa vifaa kwa wanafunzi wa Chuo Cha Ualimu Mpanda wakati wa semina ya elimu ya Hifadhi ya Jamii mkoani Katavi.
Sehemu ya wafanyakazi na wanafunzi wa Chuo cha Ufundi Stadi VETA mkoani Mpanda wakiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi kutoka SSRA wakati wa semina za elimu kwa Umma mkoani humo.

No comments: