Saturday, May 28, 2016

TEA KUENDELEA KUJENGA MABWENI YA WASICHANA NCHINI

KUELEKEA maadhimisho ya hedhi salama itakayofanyika Mei 28 , Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) imesema itaendelea kujenga mabweni na chemba za kuhifadhi na kuchomea taulo za kike ili kuwafanya wanafunzi wa kike kusoma katika mazingira mazuri.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi taulo za kike kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Yombo iliyoko wilayani Ilala, Meneja Mawasliano na Uhusiano wa TEA, Sylvia Lupembe alisema wanafunzi wa kike wamekuwa na wakati mgumu katika masomo yako kutokana na hedhi.

“ Wanafunzi wa kike wanashindwa kuhudhuria masomo kwa zaidi ya siku 80 kwa mwaka jambo ambalo linarudisha maendeleo ya mazomo yao, kwa kushirikina na wadu wa elimu tumeona tuangalie suala la kuwasaidia, hasa wale alioko kwenye shule ambazo ni vigumu kufikia,” alisema.

Alisema kwa mwaka huu wa fedha, TEA kwa kushirikiana na wadu wa elimu wanakamilisha ujenzi wa mabweni 11 ya wanafunzi wa kike hapa nchini.

Lupembe alitumia fursa hiyo kuishukuru Benki ya CRDB kwa kuwezesha kupatikana na taulo hizo za kike sambamba na mchango wao katika ujenzi wa bweni katika shule ya Sekondari Pangani ambalo limegharimu sh milioni 20.

Akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Yombo Christine Kasyupa, aliwashukuru TEA na benki ya CRDB kwa mchango wao ambao wamekuwa wkaiutoa katika shule hiyo kwani awali walishopokea dawati.

Naye Mwanafunzi Monica Singano anayesomba darasa la Saba A katika shule ya msingi Yombo, alisema msaada huyo umekuja wakati mzuri hasa kutokana na wanafunzi wengi kutoka kwenye familia mabazo hazina uwezo wa kugharamia kununua taulo za kike.

“ Wengi wa wanafunzi hapa wanatoka familia zisionauwezo wa kununua taulo za kike, wengi wanatumia vitambaa ambavyo haviwezi kuwafanya wanafunzi kukaa shule kuanzia asubuhi hadi mchana, hivyo kulazimika kwenda kubadili huku masomo yakiwa wanaendelea,” alisema
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Yombo, Christina Kasyupa wakati wa hafla ya kukabidhiwa vifaa vya kujihifadhi wanawake vilivyotolewa na Benki ya CRDB kupitia Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) kwa ajili ya wanafunzi wa shule hiyo. Kushoto ni Ofisa wa TEA, Happines Tandari, Ofisa Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), Sophia Hassad na Mwalimu Emily Salumu. (Picha na Francis Dande) 
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Yombo wakiimbo nyimbo katika hafla hiyo. 
Ofisa wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), Happines Tandari akizungumza kaba la makabidhiano ya vifaa hivyo.
Ofisa Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), Sophia Hassad (kushoto), akimkabidhi Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Yombo, Christina Kasyupa (katikati) na mwalimu Salumu sehemu ya msaada wa vifaa vya kujihifadhia wanawake ‘taulo za kike’ vilivotolewa na Benki ya CRDB kupitia Mamlaka ya Elimu Tanzania kwa ajili ya wanafunzi wa shule hiyo. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam.
Ofisa Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), Sophia Hassad (kushoto), akimkabidhi mwanafunzi wa Shule ya Msingi Yombo, Monica Singano sehemu ya msaada wa vifaa vya kujihifadhia wanawake ‘taulo za kike’ vilivotolewa na Benki ya CRDB kupitia Mamlaka ya Elimu Tanzania. Kulia ni Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Christina Kasyupa. 
Ofisa Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), Sophia Hassad (kushoto), akimkabidhi mwanafunzi wa Shule ya Msingi Yombo, Sabina Yona, sehemu ya msaada wa vifaa vya kujihifadhia wanawake ‘taulo za kike’ vilivotolewa na Benki ya CRDB kupitia Mamlaka ya Elimu Tanzania. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Christina Kasyupa.
Ofisa Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), Sophia Hassad (kushoto), akimkabidhi mwanafunzi wa Shule ya Msingi Yombo, Amina Abdalah, sehemu ya msaada wa vifaa vya kujihifadhia wanawake ‘taulo za kike’ vilivotolewa na Benki ya CRDB kupitia Mamlaka ya Elimu Tanzania. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwalimu Emily Salumu.
Ofisa Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), Sophia Hassad (kushoto), akimkabidhi mwanafunzi wa Shule ya Msingi Yombo, Rehema Baina, sehemu ya msaada wa vifaa vya kujihifadhia wanawake ‘taulo za kike’ vilivotolewa na Benki ya CRDB kupitia Mamlaka ya Elimu Tanzania. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwalimu Emily Salumu.
Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Yombo wakiwa wamenyanyua juu maboksi yaliyokuwa na vifaa vya kujihifadhi wanawake 'Taulo za kike'baada ya kukabidhiwa na Benki ya CRDB kupitia TEA.
Wanafunzi wakiwa na furaha.
Maofisa wa TEA wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule ya Msingi Yombo.

No comments: