Monday, May 16, 2016

LUHWAVI AWASILI MJINI MOSHI MKOANI KILIMANJARO, AZUNGUMZA NA WATENDAJI WOTE WA CHAMA

Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Rajab Luhwavi akipewa saluti na Kijana wa Umoja wa Vijana wa CCM wilaya ya Moshi mjini, Amiri Masawe, baada ya kuwasili mjini Moshi na kufika Ofisi ya CCM mkoa wa Kilimanjaro kuzungumza na watendaji wa Chama kutoka wilaya zote za mkoa huo leo. Wapili ni Katibu wa CCM mkoa wa Kilimanjaro Deogratius utagumirwa na watatu ni Mkuu wa Kitengo cha Utafiti na Mafunzo ya Itikadi kutoka Idara ya Itikadi na Uenezi, Makao Makuu ya CCM, Frank Uhahula.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Rajab Luhwavi akiwa na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kilimanjari Iddi Juma Mohammed baada ya kuwasili Ofisi ya CCM mkoa huo mjini Moshi leo. Kulia ni Katibu wa CCM wa mkoa huo Deogratius Rutagumirwa
Kiongozi wa Umoja wa Vijana wa CCM akiamrisha vijana kuongeza ukakamavu wakati akimkaribisha Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi Ofisi ya CCM mkoa wa Kilimanjaro mjini Moshi leo
Kiongozi wa Umoja wa Vijana wa CCM, akimpigia saluti ya kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Rajab Luhwavi kwenye Ofisi ya CCM mkoa wa Kilimanjaro mjini Moshi leo
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi alisindikizwa na Katibu wa CCM mkoa wa Kilimanjaro Deogratius Ruta, wakati akienda kuingia katika Ofisi ya CCm ya mkoa huo mjini Moshi leo
Baadhi ya viongozi wa CCM wakiwa tayari kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Rajab Luhwavi kuingia Ofisi ya CCM mkoa wa Kilimanjaro mjini Moshi, leo 
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi akiwasalimia viongozi wakati akienda kuingia katika Ofisi ya CCM mkoa wa Kilimanjaro mjini Moshi leo
"WEWE UTAKUWA KADA SAFI WA CCM" Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi akimsalimia Chipukizi, Rehema Mohammed (6), ambaye ni mtoto wa mmoja wa viongozi wa CCM waliomlaki alipokuwa akiingia katika Ofisi ya CCM mkoa wa Kilimanjaro mjini Moshi leo
"WEWE UTAKUWA KADA SAFI WA CCM" Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi akimsalimia Chipukizi, Rehema Mohammed (6), ambaye ni mtoto wa mmoja wa viongozi wa CCM waliomlaki alipokuwa akiingia katika Ofisi ya CCM mkoa wa Kilimanjaro mjini Moshi leo
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi akisaini kitabu cha wageni katika Ofisi ya Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kilimanjaro mjini Moshi leo
Katibu wa CCM mkoa wa Kilimanjaro Deogratius Rutagumirwa akiteta jambo na Mkuu wa Kitengo cha Utafiti na Mafunzo ya Itikadi kutoka Idara ya Itikadi na Uenezi Makao Makuu ya CCM, Frank Uhahula, Ofisini kwa Mwenyekiti wa CCM wa mkoa huo, walikokuwa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi akimwelekeza jambo Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kilimanjaro, Iddi Mohamed, wakati wa mazungumzo yao mafupi katika Ofisi ya CCM ya mkoa huo leo
Katibu wa CCm mkoa wa Kilimanjaro Deogratius Rutagumirwa akisoma taarifa ya mkoa huo kabla ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Rajab Luhwavi (kulia) kuzungumza na watendaji wa CCm kutoka wilaya zote za mkoa wa Kilimanjaro leo. Katikati ni Mwenyekiti wa CCM wa mkoa huo, Iddi Mohamed.
Ruta akimkabidhi taarifa Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, baada ya kuisoma
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kilimanjaro, Iddi Mohamed akifungua kikao kabla ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Rajab Luhwavi kuzungumza na watendaji wa Chama kutoka wilaya zote za mkoa wa Kilimanjaro leo
Mkuu wa kitengo cha Utafiti na Mafunzo ya Itikadi kutoka Idara ya Itikadi na uenezi Makao Makuu ya CCM, Frank Uhahula akijitambulisha na kutambulisha ugeni uliofuatana na naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Rajabu Luhwavi kwenye kikao hicho.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi akizungumza na watendaji wa Chama kutoka wilaya zote za mkoa wa Kilimanjaro, katika kikao kilichofanyika Ofisi ya CCM mkoa wa Kilimanjaro mjini Moshi leo
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi akizungumza na watendaji wa Chama kutoka wilaya zote za mkoa wa Kilimanjaro, katika kikao kilichofanyika Ofisi ya CCM mkoa wa Kilimanjaro mjini Moshi leo
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi akisisitizaa jambo, alipozungumza na watendaji wa Chama kutoka wilaya zote za mkoa wa Kilimanjaro, katika kikao kilichofanyika Ofisi ya CCM mkoa wa Kilimanjaro mjini Moshi leo. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

No comments: