Thursday, May 19, 2016

KAMPUNI YA WIA GROUP YAKABIDHI PIKIPIKI TATU KWA SERIKALI YA MTAA WA OYSTERBAY JIJINI DAR LEO.

KAMPUNI ya WIA GROUP yakabidhi msaada wa Pikipiki Tatu kwa Serikali ya Mtaa wa Oystebay jijini Dar es Salaam leo, ilikuhakikisha Ulinzi na usalama wa mtaa huo unakua imara zaidi.
Meneja mahusiano wa Kampuni ya Wia Group inayojishughulisha na masuala ya mawasiliano, Abraham Mwapongo akizungumza wakati wa kukabidhi msaada wa Pikipiki tatu kwa Serikali za mtaa wa Oysterbay jijini Dar es Salaam. Mwapongo amewaomba wadau mbalimbali washirikiane katika kuimarisha ulinzi na usalama wa mtaa wa Oysterbay kwa kutoa michango na ushirikiano kwa viongozi wa mtaa huo ili kuepusha madhara yatakayojitokeza hasa ya wizi katika jamii yao.
 Meneja mahusiano wa Kampuni ya Wia Group inayojishughulisha na masuala ya mawasiliano, Abraham Mwapongo(Katikati) akikabidhi vyeti vya manunuzi ya Pikipiki, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Oysterbay, Zefrini Lubuva(Kushoto) jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Ofisa Operesheni wa Wilaya ya Kinondoni, Inspeta Msaidizi Samwel Mkama. 
 Meneja mahusiano wa Kampuni ya Wia Group inayojishughulisha na masuala ya mawasiliano, Abraham Mwapongo (Kulia)akipongezwa na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Oysterbay, Zefrini Lubuva jijini Dar es Salaam leo mara baada ya kukabidhiwa Pikipiki Tatu na Kampuni ya Wia Group kwaajili ya kuimarisha ulizi na usalama wa mtaa wa Oysterbay.
Vijana wa ulinzi shirikishi wa mtaa wa Oysterbay wakiwa kwenye pikipiki mara baada ya kupewa pikipiki hizo ili zisaidie kurahisisha kufanya Doria malimvali katika mtaa huo. 
Ofisa Operesheni wa Wilaya ya Kinondoni, Inspeta Msaidizi, Samwel Mkama akiishukuru kampuni ya Wia Group kwa kutoa ushirikiano wa ulinzi shirikishi kwa wanamtaa wa Oysterbay jijini Dar es Salaam leo.
Amesema kuwa Kampuni hiyo iigwe mfano kwani imesaidia sana jeshi la Polisi kwani Jeshi hilo ndilo yenye jukumu la kulinda usalama wa raia pamoja na malizao. 
 Meneja mahusiano wa Kampuni ya Wia Group inayojishughulisha na masuala ya mawasiliano, Abraham Mwapongo, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Oysterbay, Zefrini Lubuva, Ofisa Operesheni wa Wilaya ya Kinondoni, Inspeta Msaidizi Samwel Mkama na  Vijana wa Ulinzi na Usalama wa Mtaa wa Oysterbay wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kampuni ya Wia Group kukaidhi pikipiki tatu kwaajili ya ulinzi na usalama wa mataa wa Oysterbay jijini Dar es Salaam leo.
Na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.

No comments: