Tuesday, April 12, 2016

Waziri Mahiga akutana na Viongozi Wakuu wa Mahakama ya MICT


Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Rais wa Mahakama ya Kimataifa ya Masalia ya kesi za Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (Mechanism for International Criminal Tribunals-(MICT) inayojengwa katika eneo la Lakilaki jijini Arusha, Mhe. Theodor Meron.

Rais huyo alifika Wizarani kwa ajili ya kujitambulisha kwa Mhe. Waziri, kumweleza maendeleo ya ujenzi wa Mahakama hiyo pamoja na kuishukuru Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano na mchango mkubwa inaotoa katika kufanikisha ujenzi huo. Pia aliipongeza Tanzania kwa kuwa mstari wa mbele katika kusimamia utawala wa sheria na haki.
Sehemu ya ujumbe uliofuatana na Mhe. Meron, Rais wa MICT.
Picha ya pamoja
Mhe. Mahiga na Mhe. Meron


Mhe. Mahiga akiagana na Mhe. Meron



...........Mkutano wa Waziri na Mwendesha Mashitaka wa MICT


Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Masalia ya kesi za Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (Mechanism for International Criminal Tribunals- (MICT), Mhe. Dkt.Serge Bremmertz. Katika mazungumzo yao Mwendesha Mashtaka huyo aliipongeza Tanzania kwa mchango wake mkubwa wa kuridhia taasisi za Umoja wa Mataifa zinazosimamia sheria kujengwa nchini na kuielezea Arusha kama makao makuu ya kimataifa ya haki kwa Ukanda wa Afrika. Pia aliahidi ushirikiano hususan katika kuwajengea uwezo wataalam wa masuala ya sheria za kimataifa hapa nchini.
Sehemeu ya Wajumbe waliofuatana na Mwendesha Mashtaka wa MICT.
Mazungumzo yakiendelea. Kushoto kwa Mhe. Mahiga ni Bw. Elisha Suku, Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa.
Mhe. Dkt. Mahiga akiagana na Mwendesha Mashtaka wa MICT, Dkt. Bremmertz.


Picha na Reginald Philip

No comments: