Thursday, April 14, 2016

Wafanyakazi wa Airtel katika Mikoa mbalimbali waitambulisha huduma ya Airtel Jipimie yatosha yako Sokoni

Wafanyakazi wa Airtel katika mikoa ya Mwanza, Arusha, Dodoma, Mbeya na Morogoro leo wameingia katika mitaa mbalimbali katika mikoa yao kuitambulisha huduma mpya ya Airtel Jipimie Yatosha yako kwa wateja na kutoa elimu jinsi ya kufurahia uhuru wa kutengeneza vifurushi vinavyokidhi mahitaji yao

Zoezi hili limefanyika jana katika mkoa wa Dar es salaam ambapo wafanyakazi wa Airtel Makao makuu waliweza kutembelia maeneo mbalimbali na kutoa elimu hiyo, halikadhalika timu ya Airtel imefikia wateja wake kupitia vyombo vya habari mbalimbali ikiwemo radio, Tv na mitandao ya kijamii kwa lengo la kuwahabarisha wateja na watanzania kwa ujumla juu ya huduma hiii ya kipekee, kibunifu na ya kwanza nchini Tanzania inayomuwezesha wateja kununua kifurushi cha muda wa maongezi tu, au kuchanganya kifurushi cha muda wa maongezi na MB za intaneti au Muda wa Maongezi na SMS lakini pia bado wanaweza kupata vifurushi vyote yaani muda wa maongezi zaidi, SMS zaidi na MB zaidi. Vifurushi hivi vinapatikana kwa siku, wiki au mwezi

Ili kujiunga na kufurushi cha Airtel jipimie yatosha yako mteja anatakiwa kupiga *149*99# kisha kufata maelekezo.
Wafanyakazi wa Airtel Mkoani Mwanza wakitoa elimu kwa wakazi Mwanza mjini na wafanyabiasharaa waendesha Bodaboda kuhusu huduma mpya ya kifurushi cha Airtel Yatosha kijulikanacho kama “Jipimie Yatosha Yako” kitakachompatia uhuru mteja kutengeneza na kununua kifurushi kinachokidhi mahitaji yake. 
Wafanyakazi wa Airtel Mkoani Mwanza wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuingia mtaani kukutana na wateja na kuitambulisha huduma mpya ya kibunifu ya Airtel jipimie yatosha yako itakayowawezesha wateja kujitengenezea vifurushi vya yatosha wanavyovitaka

Mfanyakazi wa Airtel Dodoma Abdul Hassn akiongea na mfanyakazi wa saloon katika maeneo ya Dodoma Sokoni kuhusu huduma mpya ya kifurushi cha Airtel Yatosha kijulikanacho kama “Jipimie Yatosha Yako” kitakachompatia uhuru mteja kutengeneza na kununua kifurushi kinachokidhi mahitaji yake. 

Afisa mauzo wa Airtel Dodoma Baraka Ndelele akitoa elimu kwa muuza genge katika maeneo ya Dodoma mjini juu ya huduma mpya ya kifurushi cha Airtel Yatosha kijulikanacho kama “Jipimie Yatosha Yako” kitakachompatia uhuru mteja kutengeneza na kununua kifurushi kinachokidhi mahitaji yake.
Wafanyakazi wa Airtel Mkoani Mbeya wakiitambulisha huduma mpya ya Airtel Jipimie Yatosha yako kwa wateja mtaani na kutoa elimu jinsi ya kujitengenezea na kununua kifurushi kinachokidhi mahitaji yao
Afisa masoko wa Airtel Bi Aminata Keita akimuelekeza mteja katika mkoa wa Morogoro jinsi ya kujitengenezea kifurushi chake kupita huduma ya “Jipimie Yatosha Yako” 
Wafanyakazi wa Airtel Mkoani Morogoro wakishuka kutoka kwenye basi kwenda kukutana na wateja katika maeneo yao ya kazi ili kutambulisha huduma mpya ya kibunifu ya Airtel jipimie yatosha yako itakayowawezesha wateja kutengeneza vifurushi vya yatosha wanavyovitaka
Meneja Uhusiano wa Airtel Bwana Jackson Mmbando akifanya mahojiano na Jembe radio mkoani Mwanza na kutoa elimu kwa wasikilizaji wa vipindi vyake juu ya huduma mpya ya kibunifu ya Airtel jipimie yatosha yako itakayowawezesha wateja kutengeneza vifurushi vya yatosha wanavyovitaka
Wafanyakazi wa Airtel mkoani Arusha wakiongea na wateja sokoni na kutoa elimu jkuhusu huduma mpya ya kifurushi cha Airtel Yatosha kijulikanacho kama “Jipimie Yatosha Yako” kitakachompatia uhuru mteja kutengeneza na kununua kifurushi kinachokidhi mahitaji yake.


No comments: