Saturday, April 23, 2016

WABUNGE WA BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI WAWAFAGILIA SAID SALIM BAKHRESA NA DKT. MENGI

 Mhandisi mitambo wa Azam TV, (kushoto), akiwapatia maelezo ya juu ya chumba cha uthibiti matangazo, (control room), wabunge wa EALA-Tanzania walipotembelea studio za Televisheni hiyo, Tabata jijini Dar es Salaam, Aprili 22, 2016.


NA K-VIS MEDIA/Khalfan Said
WABUNGE wa bunge la Afrika Mashariki, (EALA), kutoka Tanzania, wamewafagilia wafanyabiashara wakubwa hapa nchini, Dkt. Reginald Mengi na Mzee Said Salim Bakhresa, kwa uthubutu wao wa kutambua na kuzitumia fursa zilizopo kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki na kuwahimiza watanzania wengi kuiga mfano huo.
Pongezi hizo walizitoa Aprili 22, 2016 wakati walipotembelea studio za Azam Media, mwishoni mwa ziara yao ya kuvitembelea vyombo vya habari kwa lengo la kuhamasisha umma wa Watanzania kuchangamkia fursa kwenye Jumuiya hiyo ambayo mwenyekiti wa wabunge hao Mh. Charles Makongoro Nyerere ameiita kuwa ni jumuiya ya watu  wa Afrika Mashariki na sio ya viongozi.
“Napenda kumpongeza sana mzee Said Salim Bakhresa kwa kutambua fursa zilizopo kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki, ambapo Azam TV inaonekana kwenye nchi kadhaa wanachama wa Jumuiya lakini pia bidhaa za Azam zimesambaa karibu Afrika Mashariki na Kati, na Mzee Mengi pia anastahili pongezi kwa utambuzi wao wa fursa zilizopo kwenye Jumuiya.” Alisema Mh. Shy-Rose Bhanji, ambaye alikuwa miongoni mwa wabunge hao.
Kuna haja ya watanzania kuondokana na dhana ya kujiona wanyonge kwenye Jumuiya hii kwani wanatakiwa kuchangamkia kila fursa iliopo, mfano mimi ni mwalimu wa hisabati, ukijumlisha na Kiswahili, unaweza kupata kazi huko Sudani Kusini na maeneo mengine ya Afrika Mashariki, kwani walimu wa Kiswahili wanahitajika sana, unachopaswa ni kujiongeza tu, unakuwa na kitu kingine cha ziada.” Alisema Mh. Nderaikindo Kessy.
Kwa upande wake, Mh. Abdulla Mwinyi, alisema, wabunge wa EALA kutoka Tanzania, wamefanya jitihada hizo za kutembelea vyombo vya habari kwa kutambua mchango mkubwa unaotolewa na waandishi wa habari katika kuhabarisha umma na vyombo vya habari vinao mchango mkubwa wa kutangaza kwa kina fursa za kiuchumi kwenye Jumuiya.
Akitoa taarifa ya utendaji kazi wa kituo cha televisheni cha Azam TV, Mkurugenzi wa uendeshaji vipindi wa Azam TV,  Yahya Mohammed alisema, malengo ya Azam TV ni kufika kufanya kazi zake kwenye nchi zote za Afrika Mashariki, na Kati, ambapo kwa sasa wana soko zuri tu DRC, Rwanda, Uganda. Kenya na Burundi zinajikongoja lakini matumaini makubwa ya kulishika soko la nchi hizo yapo.


 Mh. Shy-Rose Bhanji, (kulia), na Mkuruenzi wa TV, Bi. Jane Shirima
 Mkurugenzi wa uendeshaji vipindi wa Azam TV, Yahaya Mohammed, (wa pili kushoto), akizungumza wakati akitoa taarifa yake kwa wabuneg hao
  Mkurugenzi wa uendeshaji vipindi wa Azam TV, Yahaya Mohammed, (wapili kushoto), akizungumza wakati akitoa taarifa yake kwa wabuneg hao. Wanne kulia ni Mkurugenzi wa TV, Jane Shirima

 Mkuu wa chumba cha habari Azam TV, Bw. Hassan Mhelela, akizungumza wakati wabunge hao (hawapo pichani), walipotembelea chumba cha habari
Bw. Mhelela akimpokea Mh. Shy-Rose Bhanji
 Mh. Nderaikindo Kessy
 Mh. Shy-Rose Bhanji
 Mh. Abdulla Mwinyi
 Mh. Nderaikindo Kessy
 Mh. Shy-Rose Bhanji, akipokewa na Bi. Jane Shirima
 Mh. Shy-Rose Bhanji
 Picha ya pamoja, wabunge na uongozi wa Azam TV
 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Mh. Paul Makonda, (wapili kushoto), Mh. Makongoro Nyerere, (wakwanza kushoto) Mh. Shy-Rose Bhanji (wakwanza kulia) na msanii nguli, Mrisho Mpoto, (mjomba), wakiwa kwenye picha ya pamoja kwenye chumba cha wageni Azam TV, waheshimiwa hawa walikutana. wakati Mh Mkuu wa mkoa na "mjomba" walifika kwenye mahojiano maalum kuhusu kampeni ya usafi, wabunge walifika kwa ziara ya kikazi
Wabunge wa EALA-Tanzania, kutoka kushoto, Mh. Kessy, Mh. Mwinyi, Mh. Bhanji na Mhe. Makongoro.

No comments: