Monday, April 11, 2016

UPANDISHWAJI WA MADARAJA KWA WALIMU WAZUA SITOFAHAMU ARUSHA

Na Woinde Shizza,Arusha

Baadhi ya walimu wa jiji la Arusha wamelalamikia utaratibu uliotumika wa upandishwaji wa madaraja na kusema kuwa utaratibu huo ni ujawatendea haki walimu waliofanya kazi kwa kipindi kirefu pamoja na wale ambao wamestaafu
.
Walimu hao walisema kuwa utaratibu uliotumika wa kuwachanganya walimu waliofanya kazi kwa kipindi cha mda mrefu zaidi ya miaka 20 pamoja na walimu wageni ambao wengine hawana mda mrefu kazini kwani wamefanya kwa zaidi ya mwaka mmoja hadi miaka mitatu ni mbovu na unawakatisha tama ya kufanya kazi kwa umakini.

Mmoja wa walimu hao aliyejitambulisha kwa jina la Mark Mbwabwo alisema kuwa mfumo huo wa upandishwaji wa madaraja haukuwatendea haki kabisa walimu ambao wamefanya kazi kwa kipindi cha mda mrefu kwani katika swala la ulipwaji mshahara mnakuta mwalimu aliefanya kazi kwa kipindi cha miaka 20 analipwa sawa na mwalimu ambaye amefanya kazi kwa kipindi cha mwaka mmoja au mitatu.

Gazeti hili lilitembelea ofisi ya chama cha walimu (CWT) mkoa wa Arusha ili kujua kama wamepata malamiko hayo ambayo yalitolewa na baadhi ya walimu ambao wamepandishwa madaraja na kukutana na katibu wa chama cha walimu Halmashauri ya jiji la Arusha Magreth Hovokela ambapo alitolea ufafanuzi tuhuma hizo na hatua ambazo wao kama chama cha walimu wamezifikia.

Katika ufafanuzi wake alisema kuwa swala la upandishwaji wa madaraja kwa walimu waliogota ni la mda mrefu kwani wao kama CWT walipeleka pendekezo hilo tangu December 17 mwa ka 2014 na serekali ikakubali kupandisha walimu waliogota kwa kipind cha muda mrefu , serekali ilisema kuwa walimu hao wanaopandishwa madaraja wapandishwe kutokana na muundo wa zamani ambapo ilipitishwa walimu wapandishwe kuanzia mapema July 1 ,2015 lakini swala hilo halikutekelezeka.

Aidha aliongeza kuwa swala hilo alikutekelezwa kwa kipindi hicho na lilianza kutekelezwa rasmi January 1 hadi machi mwaka huu na kila halmashauri imeshaanza kutekeleza swala hilo kutokana na ilivyojipanga pamoja na bajeti yake na katika barua ambazo walimu wamepewa za kupandishwa madaraja zinaainisha kuwa walimu hao wamepanda madaraja kuanzia January 1 mwaka huu badala ya July 7,2015 kama vile waraka unavyoelekeza.

“sasa tatizo ambalo linalalamikiwa hapa ni kwamba walimu ambao wamefanya kazi kwa muda mrefu wamepanda madaraja sawa na walimu ambao wameanza kazi hivi karibuni ,kwa mfano mwalimu ambaye alikuwa ngazi ya TGTS E₆ amepanda na kupandishwa TGTS F₆ huku alikuwa TGTS E₆ ambaye amefanya kazi kwa miaka mingi ameunganishwa na Yule ambaye anaanza kazi na wote kupewa kundi moja ambalo ni TGTS F₁ kitendo ambacho kimewavunja moyo walimu waliokaa kazini mda mrefu “alisema Magreth.

Aliongeza kuwa mbali na changamoto hiyo pia muongozi huo wa upandishwaji vyeo vya walimu wa mwaka 2015-2016 ulieleza kuwa mwalimu ambaye amekaa kazini kwa kipindi cha mda mrefu na anakaribia kustaafu apewe kipaumbele kwa kupandishwa vyeo pamoja na mshaara ili anapostaafu astaafie kwenye mshahara mpya unaoendana na daraja alilopandishwa jambo ambalo halikutekelezeka hadi baadhi ya walimu kustaafu bila kupandishwa madaraja na wamestaafia mshahara wa zamani.

“ napenda kutumia fursa hii kuiomba serekali wawape wastaafu haki yao katika madaraja walikuwa wanastaili kupanda ili kwani hawajachelewa maana hadi hivi sasa walimu waliostaafu hawajalipwa mafao yao ,kwaiyo nivyema wawapandishe madaraja ndipo waweze kuwapatia mafao yao “alisema Magret

Magret aliongeza kuwa katika halmashauri ya jiji la arusha kuna jumla ya walimu wastaafu 18 ambao walitakiwa kupandishwa madaraja lakini hawajapandishwa hadi kupelekea ukomo wa ajira zao serekalini.

Kwa kuwa hii ni serikali ya awamu ya tano ya hapa kazi tu chama cha walimu na walimu kwa ujumla wanayoimani kubwa kwa kuwa maswala yao sasa yatashulikiwa kwa wakati .

No comments: