Thursday, April 28, 2016

MONGELLA AZINDUA MRADI WA UZINDUZI WA MRADI WA UIMARISHAJI WA MIFUMO YA SEKTA ZA UMMA KATIKA MKOA WA MWANZA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella akitoa ufafanuzi wakati wa uzinduzi wa mradi wa PS3 mkoani Mwanza, kwa ajili ya kuimarisha mifumo ya Sekta ya Umma,Mh.Mongella alisema kuwa mradi huo utafanyika katika mikoa 13, ambayo itaanza na mradi huo Mwanza ni mmoja wapo.
Mkurugenzi wa TAMISEMI Bibi Betrece Kimoleta, alipokuwa akitoa maelezo kuhusu jukumu la TAMISEMI katika uzinduzi wa mradi wa PS3 mkoani Mwanza, kwa ajili ya kuimarisha mifumo ya Sekta ya Umma.

Dr. Peter Kilima, akitoa maelezo jinsi mradi utakavyo fanya kazi na afua zitakazo zingatiwa katika kutekeleza mradi huo.
Washiriki wa Uzinduzi huo kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mwanza wakiwa katika majadiliano ya Pamoja wakati wa Uzinduzi huo.( Picha zote na Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Mwanza).




Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella akitoa ufafanuzi wakati wa uzinduzi wa mradi wa PS3 mkoani Mwanza, kwa ajili ya kuimarisha mifumo ya Sekta ya Umma,Mh.Mongella alisema kuwa mradi huo utafanyika katika mikoa 13, ambayo itaanza na mradi huo Mwanza ni mmoja wapo.
Mkurugenzi wa TAMISEMI Bibi Betrece Kimoleta, alipokuwa akitoa maelezo kuhusu jukumu la TAMISEMI katika uzinduzi wa mradi wa PS3 mkoani Mwanza, kwa ajili ya kuimarisha mifumo ya Sekta ya Umma.

Dr. Peter Kilima, akitoa maelezo jinsi mradi utakavyo fanya kazi na afua zitakazo zingatiwa katika kutekeleza mradi huo.
Washiriki wa Uzinduzi huo kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mwanza wakiwa katika majadiliano ya Pamoja wakati wa Uzinduzi huo.( Picha zote na Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Mwanza)




Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella akitoa ufafanuzi wakati wa uzinduzi wa mradi wa PS3 mkoani Mwanza, kwa ajili ya kuimarisha mifumo ya Sekta ya Umma,Mh.Mongella alisema kuwa mradi huo utafanyika katika mikoa 13, ambayo itaanza na mradi huo Mwanza ni mmoja wapo.
Mkurugenzi wa TAMISEMI Bibi Betrece Kimoleta, alipokuwa akitoa maelezo kuhusu jukumu la TAMISEMI katika uzinduzi wa mradi wa PS3 mkoani Mwanza, kwa ajili ya kuimarisha mifumo ya Sekta ya Umma.

Dr. Peter Kilima, akitoa maelezo jinsi mradi utakavyo fanya kazi na afua zitakazo zingatiwa katika kutekeleza mradi huo.
Washiriki wa Uzinduzi huo kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mwanza wakiwa katika majadiliano ya Pamoja wakati wa Uzinduzi huo.( Picha zote na Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Mwanza)



HOTUBA YA MGENI RASMI, KWENYE UZINDUZI WA MRADI WA UIMARISHAJI WA MIFUMO YA SEKTA ZA UMMA KATIKA MKOA WA MWANZA
APRILI 27, 2016


Ndugu Katibu Tawala wa Mkoa,
Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya,
Ndugu Kiongozi wa Timu ya Mradi,
Mheshimiwa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Mwanza,
Waheshimiwa Wenyeviti wa Halmashauri,
Ndugu Wataalam kutoka Sekretarieti ya Mkoa,
Ndugu Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa,
Ndugu Wataalam kutoka TAMISEMI na Taasisi zingine za Serikali,
Ndugu Watendaji wa Mashirika na Taasisi za Umma na Binafsi,
Ndugu Wakuu wa Idara kutoka Mamlaka za Serikali za Mitaa,
Ndugu wana Habari,
Ndugu Wageni Waalikwa,
Mabibi na Mabwana.


Awali ya yote, napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia sisi sote afya njema na kutuwezesha kufika mahali hapa salama.  Aidha, napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Sekretarieti ya Mkoa na Timu ya Mradi wa Uimarishaji Mifumo ya Sekta za Umma kwa maandalizi mazuri ya Mkutano huu wa uzinduzi wa Mradi. Nawashukuru Wageni waalikwa wote kwa kukubali mwaliko wa kushiriki katika Mkutano huu muhimu.

Binafsi nimefarijika sana kwa kunipa heshima kubwa ya kuwa Mgeni Rasmi katika uzinduzi huu wa Mradi wa Uimarishaji Mifumo ya Sekta za Umma “Public Sector Systems Strengthening (PS3)” kwa mkoa wa Mwanza.

Ndugu Washiriki,
Mkoa wa Mwanza umekuwa na bahati kubwa ya kuwa mmoja kati ya Mikoa 13 hapa nchini ambayo itafaidika na mradi huu.  Ninafahamu kwamba mradi huu umezinduliwa katika Mikoa ya Iringa, Shinyanga, Dodoma, na Morogoro. Nimeambiwa hivi sasa Mkoa wa Mwanza unafanya uzinduzi sambamba na Mikoa ya Mbeya na Mtwara. Natoa shukrani zangu za dhati kwa Watu wa Marekani ambao ndiyo wafadhili wa Mradi huu, kupitia Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID).

Ndugu Washiriki,
Mradi huu wa Uimarishaji Mifumo ya Sekta ya Umma umeanza kwa wakati muafaka. Kama mnavyofahamu, tayari kuna juhudi kubwa zinazoendelea kufanywa na Serikali yetu chini ya Uongozi wa Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Juhudi hizi zinadhihirisha kwamba serikali ina dhamira njema ya kuhakikisha inawahudumia wananchi ipasavyo, na kwamba mifumo iliyopo Serikalini inakuwa na Tija kwa ajili ya kumsaidia mwananchi katika Taifa letu.

Serikali ya awamu ya tano imeingia madarakani kwa ari kubwa ya kuchapa kazi na juhudi kubwa zimekuwa zikifanyika katika kurekebisha mifumo tuliyo nayo hivi sasa.  Ni imani yangu kuwa Mradi huu utakuwa tija kwa utoaji wa huduma bora za Serikali kwa wananchi.

Leo tumejumuika pamoja na  Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya na Watendaji mbalimbali wa ngazi ya Mkoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa, hii ni  ishara kubwa  kuonesha kuwa kazi ambayo Mradi huu unalenga kufanya ni kubwa na muhimu kwa ajili ya Maendeleo ya Mkoa wetu wa Mwanza na Taifa kwa ujumla. Ni vizuri tukatambua umuhimu huo na kushirikiana kikamilifu na Wataalam wa mradi ili kuhakikisha kwamba lengo lililokusudiwa linafikiwa.

Ndugu Washiriki,
Kuanzia miaka ya 1990, Serikali ilikuwa ikitekeleza Maboresho katika Sekta ya Utumishi wa Umma kwa awamu mbalimbali, na katika awamu hizo, moja ya maboresho ambayo Serikali ilitekeleza ilikuwa ni Mpango wa Kurekebisha Utumishi Serikalini (Civil Service Reform Programme).  Baadhi ya mambo muhimu yaliyokuwepo kwenye mpango huo ni kuweka utaratibu ambao ungeondoa wizi wa fedha za Umma uliokuwa ukifanywa kwa njia mbalimbali kama vile kuwepo kwa Watumishi hewa.

Chini ya Programu hiyo ya kuboresha Utumishi wa Sekta za Umma, Serikali imeweka Mifumo ya Kimenejimenti kwa kusaidia kuongeza uwajibikaji katika shughuli za Serikali. Maeneo ambayo yamekuwa yakishughulikiwa, ni pamoja na uwekaji Muundo mpya wa Utumishi wa Umma, Uboreshaji utendaji kazi, Uboreshaji maslahi ya Watumishi, na Uboreshaji mifumo ya kumbukumbu, Nyaraka na taarifa za watumishi. Pia eneo lingine muhimu lililoangaliwa ni la kujengea watumishi uwezo zaidi katika kutekeleza majukumu yao ya kazi.

Ndugu washiriki,
Serikali imeanzisha Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) ambao unalenga kutoa msukumo katika utekelezaji wa mipango mbalimbali tuliyojiwekea kwa ufanisi mkubwa zaidi. Moja ya mambo yanayozungumzwa kwenye Mpango huu ni kuimarisha mifumo kwa sababu bila mifumo imara utekelezwaji wa kazi tulizojipangia hauwezi kufanikiwa.

Kwa wale wafuatiliaji wa mambo yanayoendela hapa nchini, mtakumbuka kwamba wakati Waheshimiwa Wakuu wapya wa Mikoa tulipokuwa tunaapishwa, Mhe. Rais alitupa agizo la kuhakikisha Watumishi hewa wote wanaondolewa kwenye Ankara za Mishahara ndani ya siku kumi na Tano  (15). Hii inaonyesha namna tatizo lilivyo kubwa, na namna serikali ilivyokusudia kuliondoa kabisa. Jambo hili lazima litekelezwe,  na huu ndiyo Uimarishaji wa mifumo yenyewe.

Ndugu Washiriki,
Ni muhimu tukumbuke kwamba upatikanaji wa Huduma Bora za Serikali ni haki ya kila raia wa nchi hii. Hata hivyo, ili tuweze kutekeleza kazi za Serikali za kuhudumia Wananchi kwa ufanisi, ni lazima tuwe na mifumo imara. Nimeambiwa kuwa Mradi huu unaouzinduliwa leo katika Mkoa wa Mwanza utashirikiana na Serikali na Sekta nyingine katika maeneo ya Utawala Bora na Ushirikishwaji wa Raia, Rasilimali watu, Fedha, Mifumo ya Mawasiliano, na Tafiti Tendaji.  Haya ni maeneo muhimu ambayo bila shaka yatazipa Halmashauri zetu uwezo wa kumhudumia mwananchi kwa ufanisi zaidi.

Uwepo wenu Watendaji wa ngazi ya Mkoa na Halmashaurini muhimu sana katika uzinduzi huu, kwa sababu ninyi ndio mnaotegemewa kutekeleza shughuli za Serikali katika maeneo yenu, na ndio wenye mawasiliano ya moja kwa moja na wananchi wa kawaida. 

Napenda kutoa  Rai kwa Watendaji wote wa ngazi ya Mkoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha kuwa mnatoa ushirikiano wa kutosha kwa kufanya kazi bega kwa bega na wataalam wanaoendesha Mradi huu wa Uboreshaji Mifumo ya Sekta za Umma. Kwa kutambua na kufahamu kwamba mradi huu ni wa kwetu kwa manufaa ya nchi yetu, hivyo uwajibikaji ni muhimu ili kuhakikisha kwamba mradi huu unakuwa na mafanikio makubwa.

Ndugu Washiriki,
Sisi sote tuliopo mahali hapa tunao wajibu wa kuitekeleza Falsafa ya ‘Hapa Kazi Tu’ kwa vitendo ili kuhakikisha kwamba mifumo tuliyo nayo inaboreshwa na mradi huu unafanikiwa kikamilifu. Ni matumaini yangu kuwa katika siku mtakazo kuwa hapa kujadiliana namna ya kutekeleza Mradi huu katika Halmashauri zenu, mtaandaa Mpango Kazi wa utekelezaji wa shughulina kuainisha maeneo ya vipaumbele ambayo mna uhakika kwamba ndiyo yenye tija katika kutekeleza Mradi huu kwa ushirikiano.

Mwisho,  napenda tena kutoa shukrani zangu za dhati kwa timu ya Mradi wa Uimarishaji Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) kwa utayari wao wa kuusaidia Mkoa wetu katika Mradi huu na Watu wa Marekani kupitia Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID). Karibuni sana katika Mkoa wa Mwanza.

Baada ya maelezo haya, sasa napenda kutamka kwamba Mradi huu wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma umezinduliwa Rasmi Mkoani Mwanza.

ASANTENI SANA KWA KUNISIKILIZA


No comments: