Sunday, April 3, 2016

MKUU WA WILAYA YA SHINYANGA AMSWEKA RUMANDE MHANDISI WA MANISPAA

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro amemsweka rumande Muhandisi wa halmashauri ya manispaa ya Shinyanga Simoni Ngagani, baada ya kupuuza agizo lake la kufanya maandalizi mapema ya kununua kokoto na Saruji kwa ajili ya kusimika mapipa 50 ya kutunzia uchafu kwenye mitaa mbalimbali katika manispaa ya Shinyanga ikiwemo eneo la kituo cha mabasi yaendayo wilayani. 


Tukio hilo limetokea jana asubuhi mjini Shinyanga wakati mkuu huyo wa wilaya akiwa na msafara wake alipowasili katika eneo la stendi ya mabasi yaendayo wilayani kwa lengo la kufanya uzinduzi wa kusimikwa kwa mapipa hayo na kukuta maandalizi hayajakamilika. 


Matiro alimuagiza Mhandisi huyo kufanya maandalizi hayo mapema mbele ya mkurugenzi wake wa manispaa ya Shinyanga Kalinjuna Lewis, kuwa ataandaa vifaa hivyo majira ya saa moja asubuhi ili zoezi kukusimika mapipa hayo likamilike haraka, na baada ya hapo wafanye usafi wa mazingira lakini agizo lake mhandisi huyo akapuuza. 

Mkuu huyo alipomhoji mhandisi huyo kwanini alipuuzia agizo lake la kufanya maandalizi mapema, mhandisi huyo alianza kujikanyaga kanyaga akidai sababu iliyomkwamisha ni kukosekana kwa pesa za kununua kokoto na saruji kwani mvua kubwa ilinyesha na kushindwa kwenda benki, na alivyoamka asubuhi ndipo atakafuta dhana hizo. 

Hata hivyo mkuu huyo hakuridhika na majibu hayo ndipo DC alipochukua uamuzi ya kumsweka rumande kwa kumuagiza mkuu wa kituo cha polisi wilaya ya Shinyanga kumkamata na kumuweka ndani mhandisi huyo wa ujenzi manispaa hiyo Samson Ngagani kwa kosa la kuchelewesha maandalizi ya vifaa vya ujenzi vilivyopangwa kutumika kusimika mapipa ya taka. 

“Hawezekani tukubaliane tuamke mapema ili tufanye kazi hii haraka na pia tuingie Mitaani kufanya usafi, ambapo mimi nimeamka saa 11 nikajiandaa harafu wewe una kuja saa mbili tena bila ya kufanya maandalizi yeyote hii si kunidharau hivyo naagiza OCD mkamate akakae Rumande kwanza ili liwe fundisho kwa wengine” ,alisema Matiro. 

Katika uzinduzi huo Matiro alisema mapipa hayo ya taka ambayo idadi yake ni zaidi ya 50 yatawekwa katika maeneo mbali mbali ya manispaa ya Shinyanga na wananchi wanatakiwa kuyalinda. Awali akiongea katika uzinduzi huo, mkurugenzi wa manispaa ya Shinyanga Lewis Kalinjuna alisema mapipa hayo yamepatikana kutokana na wadau mbali mbali kujitolea kuchangia baada ya kuhamasishwa na mkuu huyo wa wilaya ambapo pipa moja limegharimu shilingi elfu 90. 

Naye afisa afya wa manispaa ya shinyanga Elly Nakuzelwa alisema lengo la kuweka mapipa hayo ya taka ni kuhakikisha manispaa ya Shinyanga inakuwa katika hali ya usafi ili kuondoa magonjwa ya miripuko yanayosababishwa na uchafu ikiwemo kipindupindu. Habari na Marco Maduhu na Veronica Natalis-Malunde1 blog Angalia hapa chini picha yaliyojiri katika uzinduzi huo Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akimhoji Mhandisi wa ujenzi wa manispaa ya Shinyanga Simon Ngagani (katikati mwenye kaunda suti)kwa kupuunza agizo lake la kufanya maandalizi mapema ya kununua vifaa vya ujenzi vya kusimikia Mapipa ya uchafu 50 katika mitaa mbalimbali ya Mji wa Shinyanga ,na mwenye traksuti kushoto ni Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Kalinjuna Lewis akishuhudia Mtumishi wake akikamuliwa Jipu na hatimaye kuswekwa rumande kwa kumpuuza DC huyo-Picha zote na Marco Maduhu-Malunde1 blog Mhandisi wa manispaa ya Shinyanga Simon Ngagani akijitetea kwa mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro(kulia),kushoto ni mkurugenzi wa manispaa ya Shinyanga Lewis Kalinjuna akisikiliza utetezi wa mhandisi wake japo aliambulia kuwekwa rumande Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akiongea na wananchi kabla ya kuanza zoezi la kusimika mapipa hayo ya uchafu huku akiwaasa wayahifadhi na kutoyauza kama vyuma chakafu.

 
Mwananchi akila Miguu ya kuku kwenye zoezi la kusimika mapipa hayo huku mkuu wa wilaya ya Shinyanga akitoa elimu ya kuhifadhi mazingira kwa kutumia mapipa hayo ya uchafu. 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akichanganya zege kwa ajili ya kusimika mapipa ya uchafu Kushoto ni Mkurugenzi wa manispaa ya Shinyanga Lewis Kalinjuna akishiriki zoezi la kusimika mapipa hayo ya uchafu.

Meneja wa benki ya CRDB tawi la Shinyanga Said Pamui,ambaye ni miongoni mwa wadau waliochangia mapipa hayo akishiriki zoezi la kusimika mapipa,aliyeshikilia koleo kulia ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro.
Meneja wa benki ya CRDB tawi la Shinyanga Said Pamui,ambaye ni miongoni mwa wadau waliochangia mapipa hayo akishiriki zoezi la kusimika mapipa 
Baada ya kumaliza kuzindua zoezi la kusimika Mapipa ya uchafu, Mkuu huyo wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro alianza kukagua Mazingira ya eneo la stendi ya Mabasi ya kwenda wilayani na kukuta hali mbaya ya uchafu ,huku choo cha standi hiyo kikitisha kwa uchafu kama unavyoona kwenye picha hapo juu na hapa chini,ambapo chemba za vyoo zimeziba kwa vinyesi, hali ambayo ilimfanya mkuu huyo wa wilaya kumuagiza Mkurugenzi afanye usafi haraka ndani ya wiki moja akute pasafi Choo cha stendi ya mabasi yaendayo wilayani kikiwa kimezungukwa na uchafu yakiwemo maji machafu yaliyotuama,pichani ni afisa mazingira wa manispaa ya Shinyanga Elly Nakuzelwa akiingia katika choo hicho Mkuu wa wilaya ya Shinyanga akishuhudia uchafu katika eneo la stendi ya mabasi yaendayo wilayani mjini Shinyanga. Uchafu ukiwa katika choo cha stendi hiyo Chemba ya choo ikiwa imeziba Picha zote na Marco Maduhu-Malunde1 blog

No comments: