Sunday, April 10, 2016

MADEREVA WA MASAFA MAREFU WAANZISHIWA VITUO VYA KUPIMA AFYA ZAO


Mkuu  wa  wilaya ya  Iringa Bw  Richard Kasesela  akipima BP kwa madereva  wa masafa wakati wa uzinduzi wa kituo cha Wenda
Mwakilishi  wa Impala  Jorge Rico Grillo  akizungumza na  wanahabari

Mwakilishi wa  makampuni ya  usafirishaji Bw Arif Abri  akieleza faida ya vituo  hivyo kwa madereva
mkuu  wa mkoa  wa Iringa Bi Masenza  akijiandaa  kukata  utepe
Uzinduzi  wa  kituo  cha Ilula
Add caption
Mkuu  wa  mkoa  wa Iringa akipima BP
Na MatukuiodaimaBlog
MADEREVA  wa malori  nchini   wametakiwa  kutumia  vituo  vya upimaji virusi  vya  UKIMWI (VVU) kwa  hiari  kupima  afya   zao  katika   vituo vilivyojengwa kandokando ya barabara  kuu  ya kuanzia  Jijijini  Dar es Salaam  hadi  Tunduma mkoani  Mbeya.
Ria   hiyo   imetolewa  juzi na mwakilishi wa makampuni   ya usafirishaji mizigo Bw  Arif Abri  kutoka  kampuni ya FM Transporter  wakati wa  uzinduzi  wa Kituo  cha Ilula  wilaya ya  Kilolo na Wenda  kilichopo wilaya ya  Iringa mkoani Iringa ,kuwa matumizi    sahihi ya  vituo   hivyo itakuwa ni ukombozi mkubwa kwa madereva na  familia   zao.
Kwani  alisema   kuwa hakuna udereva salama kama madereva hawatakuwa na tabia ya kujua hali za afya zao kupitia   vituo   hivyo ambavyo  pia  madereava  hao  watavitumia  kupima na  kutibiwa   bure magonjwa  mbali mbali.
 Alisema madereva hao wakijua  afya zao  itawawezesha kufanya maamuzi ya busara yanayoweza kusaidia mikakati mbalimbali ya serikali ya kupunguza hasara na vifo vinavyotokana  vya  ajali  zinazotokana na madereva  hao  kutokuwa na afya  njema.

Hata   hivyo  alisema  pamoja  na  vituo   hivyo  kuwalenga madereva bado  wananchi wanaozunguka vituo   hivyo   wataweza  kupata   huduma  hiyo  bure na  kuwa  huduma katika  vituo   hivyo itatolewa kwa haraka  zaidi.
Huku meneja wa kampuni ya Impala Terminals Tanzania ambayo ni sehemu ya wadau hao, Jorge Rico Grillo alisema kampuni yao kwa kushirikiana na mashirika ya  Puma Energy Foundation na Trafigura walitoa fedha kwa shirika la kimataifa linalojishughulisha na afya la North Star Alliance na kujenga vituo hivyo.
Alisema pamoja na vituo hivyo viwili, wadau hao wamejenga vituo vingine vinne katika mikoa ya Dar es Salaam na Mbeya vilivyozinduliwa kwa nyakati tofauti wiki iliyopita.
Alisema lengo lao ni kuona madereva wanaotumia barabara hiyo inayokwenda hadi nchi za Malawi na Zambia wanakuwa katika mazingira rafiki yatakayowawezesha kupata ushauri na huduma mbalimbali za afya wakiwa safarini.



Mwakilishi wa shirika la North Star Alliance, John Mwachama alisema kwa kupitia vituo hivyo madereva watapata elimu ya afya, madhara ya dawa za kulevya na pombe pamoja na huduma bure ya upimaji na matibabu wa magonjwa mbalimbali ikiwemo VVU, kisukari na mengineyo jambo litakalowawezesha kuchukua tahadhari kabla na wakati wakitumia barabara hiyo.
Meneja Uendeshaji wa Puma Energy Tanzania, Lameck Hiliyai alisema kujengwa kwa vituo hivyo kutasaidia makampuni ya usafirishaji kuwatumia madereva wanaojali afya zao.
Akizindua vituo hivyo, Mkuu wa Mkoa wa Iringa alisema vituo hivyo vitakuwa vya manufaa sana kwa madereva na wananchi walio jirani navyo kwani vinaongeza upatikanaji wa huduma zinazotolewa pia katika vituo vingine binafsi na vya serikali.Kwa upande  wake  mkuu  wa mkoa   wa Iringa, Amina Masenza  akizindua vituo hivyo alipongeza wadau hao kwa  kujitolea  kujenga  vituo  hivyo na  kutaka watendaji wa  vituo   hivyo  kufanya kazi kwa uaminifu mkubwa badala ya  kuanza  kuiba madawa.
Vituo hivyo ambavyo pia vitatoa huduma kwa wananchi wanaovizunguka, vimejengwa katika mji mdogo wa Ilula, wilayani Kilolo na kijiji cha Wenda, Iringa Vijijini kwa msaada wa wadau wa sekta ya usafirishaji nchini watakaogharamia uendeshaji wake hadi mwaka 2018.

No comments: