Sunday, April 17, 2016

DARAJA LA KIGAMBONI KUFUNGULIWA RASMI JUMANNE APRILI 19, 2016


Viongozi Shrika la Taifa Hifadhi ya Jamii NSSF wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wakandarasi wa daraja la Kigamboni wakati lilipofunguliwa kwa ajili ya kupita magari kupita bure huku watembea kwa miguu na waendesha baiskeli wakipita bure. Daraja hilo litazinduliwa rasmi na Rais Dk. John Magufuli Jumanne tarehe 19.4.2016. 
Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja la Kigamboni, Karim Mataka akiwa katika eneo la daraja la Kigamboni mara baada ya kufunguliwa kwaajili ya kupita magari na waenda kwa miguu.
Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja ala Kigamboni, Karim Mataka (katikati) akionyesha barabara za kuingilia darajani upande wa Kigamboni.
Maeneo ya kuingilia darajani na kulipia tozo katika daraja la Kigamboni upande wa Kigamboni.
Ofisi mbalimbali zilizopo katika daraja la Kigamboni kikiwepo Kituo cha Polisi.
Magari yakipita kwa mara ya kwanza katika daraja la Kigamboni bila kulipa tozo.
Muonekano wa daraja la Kigamboni baada ya magari kuanza kupita.
Meya wa wa jiji la Dar es Salaam, Issa Mwita Charles akipata maelezo kutoka kwa Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja la Kigamboni, Karim Mataka wakati alipopita katika daraja hilo siku ya kwanza baada ya kufunguliwa kwa daraja hilo.
Magari yakipita.
Meya wa wa jiji la Dar es Salaam, Issa Mwita Charles akiwa katika picha ya pamoja na Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja ala Kigamboni, Karim Mataka.
Meya wa wa jiji la Dar es Salaam, Issa Mwita Charles akiagana na Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja ala Kigamboni, Karim Mataka walipokutana wakati akipita katika daraja hilo siku ya kwanza baada ya kufunguliwa kwa watumiaji.
Waenda kwa miguu wakipita katika daraja hilo.
Eneo lililoandaliwa kwa ajili ya kuweka jiwe la msingi wakati wa uzinduzi rasmi.
Pikipiki na magari yakipita darajani.
Magari yakielekea upande wa Kigamboni.
Waendesha baiskeli nayo wakipita.
Wengine wakishangaa darajani.
Watu wakipita darajani.
Mandhari ya darajani.

No comments: