Friday, April 22, 2016

BENKI YA CRDB YATOA MSAADA WA MIFUKO 70 YA SARUJI KWA SHULE YA SEKONDARI KIBASILA KUSAIDIA UKARABATI WA UZIO.

Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Quality Center, Clementina Kinabo (wa pili kulia), ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mahafali ya 15 ya Kidato cha Sita katika Shule ya Sekondari Kibasila akiwasili shuleni hapo, Kulia ni Mkuu wa shule hiyo, Yasinta Matilya. Benki ya CRDB ilitoa msaada wa mifuko 70 ya saruji kwa ajili ya ukarabati wa uzio wa shule hiyo katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
 (Picha na Francis Dande)
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Kibasila wakiimba wimbo wa Taifa.
Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Quality Center, Clementina Kinabo (kushoto), akipokea risala kutoka kwa Emmanue Moah ambaye ni mwanafunzi wa Kidato cha Sita wa Shule ya Sekondari Kibasila wakati mahafali ya 15 ya shule hiyo jijini Dar es Salaam. Benki ya CRDB ilikabidhi mifuko 70 ya saruji kwa ajili ya ukarabati wa uzio wa shule hiyo
Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Quality Center, Clementina Kinabo (kulia), akikabidhi mifuko 70 ya saruji kwa Mkuu wa Shule ya Sekondari Kibasila, Yasinta Matilya kwa ajili ya ukarabati wa uzio wa shule hiyo.
Mkuu wa Shule ya Sekondari Kibasila, Yasinta Matilya (kulia), akimshukuru Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Quality Center, Clementina Kinabo baada ya mifuko 70 ya saruji.
Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Quality Center, Clementina Kinabo na Mkuu wa Shule ya Sekondari Kibasila, Yasinta Matilya wakikagua mifuko ya saruji iliyotolewa na Benki ya CRDB.
Maktaba ya Shule. 
Wanafunzi wakiwa na furaha.
Wanafunzi wakiwa na furaha ya kumaliza masomo yao ya Kidato cha Sita.
Meza Kuu.
Mkuu wa Shule ya Sekondari Kibasila, Yasinta Matilya akizungumza katika mahafali hayo.
Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Quality Center, Clementina Kinabo akizungumza katika mahafali hayo. Kushoto ni Principal Public Relations Officer wa Benki ya CRDB, Willy Kamwela.
Principal Public Relations Officer wa Benki ya CRDB, Willy Kamwela (wa pili kulia), akiwa katika mahafali hayo. 
Wanafunzi wakiimba nyimbo za kuwaaga wenzao wakati wa mahafali yao.
Wanafunzi wakiwa katika mahafali hayo.
Wanafunzi wakiwa katika mahafali hayo.

Wazazi pamoja na wanafunzi wakiwa katika mahafali hayo.

No comments: