Friday, March 18, 2016

TASAF yapatiwa Dola milioni 665 kunusuru kaya masikini

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile (kulia) akibadilishana mkataba wa makubaliano na Mwenyekiti wa Wadau wa Maendeleo nchini ambaye pia ni Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia anayesimamia nchi za Tanzania, Burundi, Malawi na Somalia Bi. Bella Bird (kushoto) mara baada ya kusaini makubaliano ya jumla ya Dola za Kimarekani milioni 665 zilizotolewa na Wadau hao ili kusaidia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) katika Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini nchini.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile akisaini mkataba wa makubaliano wa jumla ya Dola za Kimarekani milioni 665 zilizotolewa na Wadau wa Maendeleo nchini ili kusaidia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) katika Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini nchini.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile (kulia) akiongea na wadau wa maendeleo mara baada ya kusaini mkataba wa makubaliano wa jumla ya Dola za Kimarekani milioni 665 zilizotolewa na Wadau wa Maendeleo ili kusaidia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) katika Mpango wake wa Kunusuru Kaya Masikini nchini. Kushoto ni Mwenyekiti wa Wadau wa Maendeleo nchini ambaye pia ni Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia anayesimamia nchi za Tanzania, Burundi, Malawi na Somalia Bi. Bella Bird.
Mwenyekiti wa Wadau wa Maendeleo nchini ambaye pia ni Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia anayesimamia nchi za Tanzania, Burundi, Malawi na Somalia Bi. Bella Bird jijini Dar es slaam. Kulia ni Katibu Mkuu Wiazara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Ladislaus Mwamanga akiwashukuru Wadau wa Maendeleo nchini na kuwaahidi kuwa fedha walizotoa zitatumika kwa malengo yaliyowekusudiwa ili kuwasaidia Watanzania wanaoishi katika hali ya maisha duni waweze kupata mahiji yao ya kila siku.
Wadau wa Maendeleo wakimskiliza Mwenyekiti wa Wadau wa Maendeleo nchini ambaye pia ni Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia anayesimamia nchi za Tanzania, Burundi, Malawi na Somalia Bi. Bella Bird wakati wa mkutano jijini Dar es salaam.
Baaadhi ya waandishi wa habari (waliosimama) wakiendelea na kazi yao wakati wa hafla ya kusaini mkataba wa makubaliano wa jumla ya Dola za Kimarekani milioni 665 zilizotolewa na Wadau wa Maendeleo nchini ili kusaidia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) katika Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini nchini.
Kaimu Mkurugenzi Shirika la Misaada la Marekani (USAID) Daniel Moore (kushoto) akiteta jambo na Katibu Mkuu Wiazara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile (kulia) mara baada ya hafla ya kusaini mkataba na wadau wa maendeleo jijini Dar es salaam ili kusaidia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) katika kutekeleza Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini nchini.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile (wa pili kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Wadau wa Maendeleo nchini. Wa pili kulia ni Mwenyekiti wa Wadau wa Maendeleo nchini ambaye pia ni Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia anayesimamia nchi za Tanzania, Burundi, Malawi na Somalia Bi. Bella Bird na Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Ladislaus Mwamanga (wa kwanza kulia). (Picha na Eleuteri Mangi-MAELEZO).

Serikali ya Tanzania imesaini mkataba wa makubaliano wa jumla ya Dola za Kimarekani milioni 665 na Wadau wa Maendeleo ili kusaidia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) katika Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini nchini.

Mkataba huo ambao umetiwa saini jijini Dar es Salaam unawataka watendaji kuweka utaratibu ambao unaenda sambamba na Mpango wa utekelezaji bila kuingilia majukumu ya mamlaka ya Serikali katika utekelezaji wa TASAF wa kunusuru kaya masikini.

Akizungumzia mkatraba huo mara baada ya kusaini kwa niaba ya Serikali ya Tanzania, Katibu Mkuu Wiazara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile amesema kuwa mpango huo unaosimamiwa na TASAF unalenga kuziwezesha kaya masikini nchini kujiongezea kipato na kupata chakula cha kutosha pamoja na kujiletea maendeleo yao wenyewe.

Katika kutekeleza mpango huo wa TASAF uwe wa tija kwa kaya masikini kulingana na malengo tarajiwa, mpango umegawanyika katika maeneo makuu manne ambayo yanatarajiwa kuboresha hali za watu wanaoishi katika hali duni nchini.

Maeneo hayo yanayotekelezwa ni pamoja na kuhawilisha fedha kwa kaya masikini hasa zile zenye watoto ili ziweze kupata huduma za elimu kwa kuwawezesha watoto walio katika shule za msingi na sekondari kupata mahitaji muhimu shuleni pamoja na kupata huduma za afya na kuongeza kipato kwa kaya masikini kupitia uwekaji akiba na shughuli za kiuchumi.

Maeneo mengine ya utekelezaji huo ni kutoa ajira ya muda kwa kaya masikini zenye watu wenye uwezo wa kufanya kazi wakati wa kipindi cha njaa na majanga yakiwemo ukame na mafuriko pamoja na kujenga uwezo katika ngazi zote za uteklelezaji wa kutoa mafunzo yatakayoboresha utekelezaji wake.

Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini  nchini umekuwa na mafanikio nchini ambapo hadi sasa umeshahawilisha kwa walengwa mizunguko 14 ya malipo ya jumla ya fedha zote  zilizohawilishwa kufikia bilioni Sh. 224 na kuandikisha kaya milioni 1.1 tangu uanzishwe  mwaka 2012 na kuhudumia halmashauri 159 Tanzania Bara pamoja na halmashauri 11 Tanzania Zanzibar.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Wadau hao wa Maendeleo nchini ambaye pia ni Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia anayesimamia nchi za Tanzania, Burundi, Malawi na Somalia Bi. Bella Bird amesema kuwa makubaliano yaliyotiwa saini yataboresha uhusiano na kuendeleza majadiliano baina ya Serikali na wadau kuhusu kunusuru kaya masikini na kutoa msaada wa kitaalamu utakaohitajika ili kufikia malengo yanayotarajiwa.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Ladislaus Mwamanga amewahakikishia wadau hao wa maendeleo kuwa fedha walizotoa kwa mfuko huo zitatumika kwa malengo yaliyowekwa ili kuwasaidia Watanzania wanaoishi katika hali duni waweze kuinua hali zao kiuchumi na kupata mahiji yao ya kila siku.

Wadau waliotia saini mkataba huo wa makubaliano ya kunusuru kaya masikini ni pamoja Benki ya Dunia, Ubalozi wa Sweden, Shirika la Maendeleo la Uingereza (DFID), Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mtaifa (UNDP), Shirika la Misaada la Marekani (USAID), Shirika la Watoto la Umojas wa Mtaifa (UNICEF), Shirika la Kazi Duniani (ILO) na Shirika la Watu wa Umoja wa Mataifa (UNFPA), Wizara ya Fedha na Mipango na TASAF kwa upande wa Tanzania.

No comments: