Saturday, March 5, 2016

Tamasha la Michezo la Wanawake kuelekea kilele cha siku wa wanawake duniani lafana

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (watatu kulia) akiongoza wanawake kufanya mazoezi wakati wa tamasha la maadhimisho kuelekea kilele cha siku ya wanawake katika viwanja vya Uhuru leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Bibi. Sihaba Nkinga.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Bibi. Sihaba Nkinga (katikati) akifanya mazoezi ya kukimbia wakati wa tamasha la maadhimisho kuelekea kilele cha siku ya wanawake katika viwanja vya Uhuru leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mjumbe wa Baraza la Michezo ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Rungwe Bibi. Zainabu Mbussi.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akiongea na wanawake (hawapo pichani) walioudhuria tamasha la maadhimisho kuelekea kilele cha siku ya wanawake katika viwanja vya Uhuru leo jijini Dar es Salaam.
Makamu Mwenyekiti Baraza la Michezo Taifa Bibi. Zaynab Matitu Vulu ambaye pia ni Mbunge Viti Maalum Mkoa wa Pwani akimkaribisha mgeni rasmi Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama wakati wa tamasha la maadhimisho kuelekea kilele cha siku ya wanawake katika viwanja vya Uhuru leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akirusha mpira kuashiria ufunguzi wa mchezo wa mpira wa pete wakati wa tamasha la maadhimisho kuelekea kilele cha siku ya wanawake katika viwanja vya Uhuru leo jijini Dar es Salaam. Anayezuia mpira ni Mjumbe wa Baraza la Michezo ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Rungwe Bibi. Zainabu Mbussi.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (wapili kushoto) akipata maelekezo kuhusu michezo mbalimbali iliyoandaliwa kutoka kwa Kaimu Katibu Mtendaji Baraza la Michezo la Taifa Bw. Mohamed Kiganja (wapili kulia) wakati wa tamasha la maadhimisho kuelekea kilele cha siku ya wanawake katika viwanja vya Uhuru leo jijini Dar es Salaam.
Wanamichezo kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wakifanya mazoezi ya viungo kabla ya kushiriki michezo mbalimbali wakati wa tamasha la maadhimisho kuelekea kilele cha siku ya wanawake katika viwanja vya Uhuru leo jijini Dar es Salaam.
Wanamichezo kutoka Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF), wakijiandaa kushiriki mchezo wa kuvuta kamba ambapo walishindana na Wanamichezo kutoka Wizara Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo tamasha la maadhimisho kuelekea kilele cha siku ya wanawake katika viwanja vya Uhuru leo jijini Dar es Salaam.
Wanamichezo kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wakiwavuta wapinzani wao kutoka Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) mbalimbali wakati wa tamasha la maadhimisho kuelekea kilele cha siku ya wanawake katika viwanja vya Uhuru leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akikagua timu ya mpira wa miguu kutoka Shule ya Sekondari Makongo ambao walishiriki tamasha la maadhimisho kuelekea kilele cha siku ya wanawake katika viwanja vya Uhuru leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akipokea fomu ya kujiunga kwa hiari katika Mfuko wa Hiara wa PSPF kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa PSPF Bw. Adam Mayingu wakati wa tamasha la maadhimisho kuelekea kilele cha siku ya wanawake katika viwanja vya Uhuru leo jijini Dar es Salaam.
Mgeni rasmi (katikati mstari wa mbele) Mhe. Jenista Mhagama akiwa katika picha ya pamoja washiriki na wadau waliondaa tamasha la maadhimisho kuelekea kilele cha siku ya wanawake katika viwanja vya Uhuru leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi wa wanafunzi wakifuatilia michezo mbalimbali iliyokua ikiendelea wakati wa tamasha la maadhimisho kuelekea kilele cha siku ya wanawake katika viwanja vya Uhuru leo jijini Dar es Salaam.








Matukio ya michezo mbalimbali wakati wa tamasha la maadhimisho kuelekea kilele cha siku ya wanawake katika viwanja vya Uhuru leo jijini Dar es Salaam. Picha na: Beatrice Lyimo na Genofeva Matemu

No comments: