Thursday, March 3, 2016

MAKAMU WA RAIS AZINDUA SALA MAALUM YA KULIOMBEA TAIFA NA AUNGUA MKUTANO WA WABUNGE WA BUNGE LA AFRIKA LEO.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katikati, akiwa na viongozi wa Mtandao wa Kingdom Leadership Tanzania Network na Viongozi wa Dini wa Mataifa mbalimbali Duniani, wakati wa uzinduzi wa mpango wa Sala maalum ya kuliombea Taifa utakaofanyika kila mwaka, uzinduzi huo umezinduliwa leo March 03, 2016 katika Hoteli ya Hayyat jijini Dar es salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na baadhi ya Viongozi wa Mtandao wa kitaifa wa Kingdom Leadership Network Tanzania na viongozi wa Dini wa Mataifa mbalimbali Duniani wakati wa uzinduzi wa mpango wa Sala maalum ya kuliombea Taifa utakaofanyika kila mwaka, uzinduzi huo umezinduliwa leo March 03, 2016 katika Hoteli ya Hayyat jijini Dar es salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akifungua mkutano wa tisa wa siku mbili kwa Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki pamoja na Wabunge wa Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, unaojadili kuhusu kupitia kanuni, Sheria na Itifaki zilizotolewa na Jumuiya ya Afrika Mashariki juu ya Chaguzi zinazofanyika ndani ya Nchi hizo. Mkutano huo umefunguliwa leo katika ukumbi wa LAPF Makumbusho jijini Dar es salaam
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katikati, akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Mtandao wa Kitaifa wa Kingdom Leadership Tanzania Network na Viongozi wa Dini wa Mataifa mbalimbali Duniani baada ya uzinduzi wa Mpango wa Sala Maalum ya kuliombea Taifa uliofanyika leo March 03,2016 katika Hoteli ya Hayyat Dar es salaam.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe. Sheyros Banji nje wa ukumbi wa LAPF Makumbusho jijini Dar es salaam leo March 03,2016 baada ya kufungua mkutano wa tisa wa siku mbili kwa Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki pamoja na Wabunge wa Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, unaojadili kuhusu kupitia kanuni, Sheria na Itifaki zilizotolewa na Jumuiya ya Afrika Mashariki juu ya Chaguzi zinazofanyika ndani ya Nchi hizo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika picha ya pamoja na wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki pamoja na Wabunge wa Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki baada ya kufungua mkutano wa tisa unaojadili kuhusu kupitia kanuni, Sheria na Itifaki zilizotolewa na Jumuiya ya Afrika Mashariki juu ya Chaguzi zinazofanyika ndani ya Nchi hizo.mkutano huo umefunguliwa leo Marchi 03,2016 katika ukumbi wa LAPF Makumbusho jijini Dar es salaam. 
(Picha na OMR)

No comments: