Wednesday, February 24, 2016

MAKAMU WA RAIS, SAMIA SULUHU AZINDUA MPANGO WA KUWAONGEZEA UWEZO WANAWAKE LEO JIJINI DAR ES SALAAM.

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amezindua Programe maalum ya Mwanamke na wakati ujao (Female Future) ambayo itawajengea uwezo wanawake katika bodi za wakurugenzi wa taasisi na makampuni mbalimbali.

Uzinduzi huo uliofanyika leo katika Hoteli ya Hyatt Regency  jijini Dar es Salaam leo na kuhudhuliwa na watu mbalimbali wakiwepo wakenya, waganda na watanzania na watu kutoka bara la Ulaya na Asia.

Makamu wa Rais, Samia Suluhu amesema kuwa wanawake ni watendaji wazuri na wanamaamuzi mazuri katika uongozi na uendelezaji wa makamuni pamoja na Tasisi mbalimbali.

Mpango huo uliozinduliwa leo umefanywa wanachana chama cha  waajili Tanzania ambao unalenga kuwajengea uwezo wanawake ili kuongeza ufanisi katika biashara zao na kujenga mtandao ambao utaongeza juhudi na maarifa kwa wanawake.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza wakati wa kuzindua Programe maalum ya Mwanamke na wakati ujao (Female Future) ambayo itawajengea uwezo wanawake katika bodi za wakurugenzi wa taasisi na makampuni mbalimbali iliyofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Hyatt Regency  jijini Dar es Salaam leo.
Makamu Mwenyekiti wa kampuni ya ATE, Zuhura Muro akizungumza na wanawake kutoka kutoka makampuni mbalimbali leo wakati Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizindua mpango malumu wa kuwafundisha wanawake ili waweze kuwa na uwezo wa kuleta mawazo yenye kuinua kampuni au taasisi mbalimbali kuwa kubwa.
Mtumbuizaji akitumbuiza katika uzinduzi wa mpango wa kuinua wanawake katika uongozi wa juu katika makampuni au taasisi mbalimbali, uzinduzi  huo umefanyika leo katika hoteli Hyatt Regency jijini Dar es Salaam. 
 Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya NMB, Ineke Bussemaker akitoa ushuhuda alioufanya katika taasisi hiyo ya fedha kwa maendeleo ya wanawake waliokusanyika leo ili kuzindua mpango wa kuwaundisha wanawake uongozi katika makampuni na Tasisi mbalimbali katika uzinduzi uliofanyika leo katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam leo.
Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu, sera na Uratibu wa bunge, Jenister Mhagama akizungumza leo katika uzinduzi wa Programe maalum ya Mwanamke na wakati ujao (Female Future) ambayo itawajengea uwezo wanawake katika bodi za wakurugenzi wa taasisi na makampuni mbalimbali iliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Hyatt Regency  jijini Dar es Salaam leo.
Wadau mbalimbali wakisikiliza shuhuda mbalimbali za wadau wa uongozi kwa wanawake kutoka hapa nchini, Uganda na Kenya leo katika uzinduzi wa Programe maalum ya Mwanamke na wakati ujao (Female Future) ambayo itawajengea uwezo wanawake katika bodi za wakurugenzi wa taasisi na makampuni mbalimbali iliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Hyatt Regency  jijini Dar es Salaam
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiteta jambo na Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu, sera na Uratibu wa bunge, Jenister Mhagama leo katika uzinduzi wa Programe maalum ya Mwanamke na wakati ujao (Female Future) amayo itawajengea uwezo wanawake katika uongozi wa juu wa taasisi na makampuni mbalimbali katika uzinduzi uliofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency  jijini Dar es salaam leo. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika picha ya pamoja baada ya kuzindua Programe maalum ya Mwanamke na wakati ujao (Female Future) katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es salaam leo.

Picha na Avila Kakingo wa Globu ya Jamii.

No comments: