Tuesday, January 26, 2016

MADAKTARI BINGWA KUTOKA CHINA WAKISHIRIKIANA NA MADAKTARI WA ZANZIBAR WATOA HUDUMA ZA MATIBABU KWA WANANCHI WA KIJIJI CHA MATEMWE UNGUJA.

 Dokta Abdull Maulid Abdull akimpima Miwani ya kuonea Mwananchi Chale Muumin Fumu mkaazi wa Kijiji cha Matemwe Tunda ngaa katika matibabu yalio fanyika skuli ya matemwe mkoa wa Kaskazini unguja.
 Dokta Rajab Mohd Haj akimkagua Jicho Mzee Muhidin M Ali Mkaazi wa Kijiji cha Matemwe katika matibabu yaliofanyika Skuli ya Matemwe Mkoa wa Kaskskazini Unguja.
 Dokta Fei Jie kutoka China akimpima Masikio Bi Fatma Khamis Jaku mkaazi wa Kijiji cha Matemwe Mfuruni katika matibabu yalio fanyika Skuli ya Matemwe Mkoa wa Kaskazini Unguja.
 Mtoto Iddi Khamis Juma akipatiwa huduma ya kupimwa uzito.
 Daktari Bingwa kutoka China Yun Lai Gao kushoto na Mwanafunzi kutoka Zanzibar School of Health Machano M Ali kwa pamoja wakipata maelezo kutoka kwa Mgonjwa anaesumbuliwa na maradhi ya Ganzi Haji Ali Mcha kabla ya kumtibu huko Skuli ya Matemwe.
 Dokta Yu Lu akimgonga ngumi Mgonjwa anaesumbuliwa na maradhi ya Mgongo Mkadam Vuai kwaajili ya kumpatia matibabu ambayo yamekua yakimsumbua kwa muda mrefu.
 Mwandishi wa habari wa Star TV Abdalla Pandu akimuhoji Mwanchi wa Kijiji cha Matemwe Mbupurini Chida Pili Khamis Juu ya Huduma za Afya zilizowafikia katika kijiji chao cha Matemwe Mkoa wa Kaskazini Unguja. Picha na Abdalla Omar-Maelezo Zanzibar.

No comments: