Tuesday, January 5, 2016

DKT. SHEIN AWEKA JIWE LA MSINGI WODI YA WATOTO NA UPANUZI WA HOSPITALI YA MNAZI MMOJA(ORIO)

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Mkandarasi wa Wizara ya Afya Mathna Kassim Marine (kushoto) baada ya kuweka jiwe la msingi Upanuzi wa Hospitali ya Mnazi Mmoja (ORIO) leo ikiwa ni katika shamra shamra miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar (katikati) Mkandarasi wa ujenzi kampuni ya Rans Ali Nassor Salim.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akifungua pazoakama ishara ya uwekaji wa jiwe la msingi Wodi ya Watoto katika Hospitali ya Mnazi Mmoja leo ikiwa ni katika shamra shamra miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akitoa Ushauri kwa Uongozi wa Hospitali wa Wizara ya Afya wakati alipokuwa akitembelea hatua ya ujenzi Wodi ya Watoto na upanuzi wa Hospitali ya Mnazi Mmoja baada ya kuweka jiwe la msingi miradi hiyo miwili leo ikiwa ni katika shamra shamra miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar,(kushoto) ni Mkandarasi wa ujenzi kampuni ya Rans Ali Nassor Salim.
Baadhi ya wanafunzi wa Vyuo mbali mbali vya Afya wakiwa katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi Wodi ya Watoto na upanuzi wa Hospitali ya Mnazi Mmoja leo ikiwa ni katika shamra shamra miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Baadhi ya madaktari na Maafisa wa Hospitaliya mnazi mmoja wakiwa katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi Wodi ya Watoto na upanuzi wa Hospitali ya Mnazi Mmoja leo ikiwa ni katika shamra shamra miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Viongozi na wegeni mbali mbali walioalikwa katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi Wodi ya Watoto na upanuzi wa Hospitali ya Mnazi Mmoja leo ikiwa ni katika shamra shamra miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein alipokuwa akitoahutuba yake ya uwekaji wa jiwela msingi mradi huo.
Balozi wa Uholanzi Nchini Tanzania Bw.Jaap Frederiks alipokuwa akitoa salamu zake mbele ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi Wodi ya Watoto na upanuzi wa Hospitali ya Mnazi Mmoja leo ikiwa ni katika shamra shamra miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar
Naibu Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo akimkaribisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein kutoa nasaha zake kwa wananchi pamoja na wafanyakazi wa Hospitali ya mnazi mmoja katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi Wodi ya Watoto na upanuzi wa Hospitali ya Mnazi Mmoja leo ikiwa ni katika shamra shamra miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akitoa nasaha zake kwa wananchi pamoja na wafanyakazi wa Hospitali ya mnazi mmoja katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi Wodi ya Watoto na upanuzi wa Hospitali ya Mnazi Mmoja leo ikiwa ni katika shamra shamra miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar(kulia) Naibu Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo na Balozi wa Uholanzi Nchini Tanzania Bw.Jaap Frederiks.[Picha na Ikulu.]

No comments: