Tuesday, December 15, 2015

MSHINDI WA SHINDANO LA MAMA SHUJAA WA CHAKULA 2015 CAROLINE CHELELE, AKABIDHIWA RASMI ZAWADI ZA VIFAA VYA KILIMO

Mshindi wa Shindano la Mama shujaa wa Chakula Msimu wa nne Bi. Caroline Chelele aliyekaa kwenye Pawatila akifurahia zawadi zake, Muda mfupi baada ya kukabidhiwa.
 Katibu Tawala wa Wilaya ya Kilombelo Bw. Yahya Naiya (wa pili kushoto) aliye muwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Kilombelo akikata utepe kuashiria tukio la kumkabidhi zawadi rasmi mama shujaa wa chakula msimu wa nne 2015 Bi. Caroline Chelele, wa kwanza kushoto ni Mercy Minja Kaimu mkurugenzi wa wa mji wa Ifakara, wa tatu kutoka kulia ni Mama Shujaa wa Chakula Bi. Caroline Chelele na Mbunge wa Jimbo la Kilombelo Mh. Peter Lijuakali
 Katibu Tawala wa Wilaya ya Kilombelo Bw. Yahya Naiya (wa pili kushoto) aliye muwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Kilombelo akimpongeza Mama shujaa wa chakula 2015 baada ya kukabidhiwa zawadi ya vifaa vya kilimo vyenye thamani ya Tsh Milioni Ishirini(20,000,000)
 Vifaa  vya kilimo ambavyo alikabidhiwa  mama Shujaa wa Chakula Msimu wa nne 2015, ikiwa ni Pawatila na Mashine ya kumwagilia na Shamba lenye Hekta 7 ambalo halipo pichani.
 Mshindi wa Shindano la Mama shujaa wa chakula linalo endeshwa na Oxfam kupitia Programu yake ya Grow Bi Caroline Chelele akitoa neno la Shukurani baada ya kukabidhiwa zawadi.
 Katibu Tawala wa Wilaya ya Kilombelo Bw. Yahya Naiya (wa pili kushoto) aliye muwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Kilombelo, akitoa neno la shukurani kwa Shirika la Oxfam kwa jinsi wanavyo wajali na kuwawezesha wakulima wadogo wadogo.
Mbunge wa Kilombelo Mh. Peter Lijuakali akimpa pongezi mama shujaa wa Chakula 2015 kwa kuleta ushindi mkubwa wilayani hapo na kuwasihi akinamama wengine wajitokeze kushiriki kipindi ambacho nafasi inatokea tena na kurudisha ushindi huko.
Meneja wa Ushawishi na utetezi kutoka Oxfam Eluka Kibona akielezea kwa undani kuhusiana na shindano la Mama shujaa wa Chakula.
Mtaalam wa Kilimo hai kutoka SOAM wa tatu kutoka kushoto akitoa maelezo ya namna ya kutengeneza mbolea asiyo na kemikali yoyote kwa kutumia Majani,Magugu, Majivu,Maji na Udongo
Baadhi ya wanakijiji wakifanya kazi kwa vitendo kwa kusombelea nyasi kavu pamoja na magugu kwa ajili ya kutengeneza Biwi
Shamba darasa la utayarishaji wa Biwi likiwa linaendelea 
Baadhi ya wanakijiji ambapo mama Shujaa wa Chakula alipokabidhiwa zawadi zake, wakifuatilia kwa makini shamba Darasa
 Mshindi wa shindano la Mama Shujaa wa chakula 2015 msimu wa nne Bi. Caroline chelele (Kulia) akimkabidhi zawadi Kaimu Mkurugenzi wa Mji wa Ifakara Bi. Mercy Minja kwa niaba ya Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombelo
 Bi.Caroline chelele akikabidhi zawadi yake ya Kigoda kwa Shirika la Oxfam, kutoka kushoto ni Narsis Silvesti, Eluka Kibona na wa kwanza kulia ni Suhaila Thawer wote kutoka Oxfam Tanzania
 Mama Shujaa wa chakula akikabidhi zawadi ya Picha kwa Shirika la Oxfam
 Watalam wa Kilimo hai kutoka SOAM wakimkabidhi vipeperushi vinavyozungumzia kilimo hai Mama Shujaa wa Chakula 2015 Bi. Caroline Chelele
 Baadhi ya wananchi waliokuwa katika sherehe hizo za kukabidhiwa zawadi mama shujaa wa Chakula.
Picha ya pamoja ya viongozi wa Wilaya ya Kilombelo, Shirika la Oxfam na Mshindi wa Shindano la Mama shujaa wa Chakula Msimu wa nne 2015 Bi.Caroline Chelele
 ………………………………………………………………………………………………. 
Mshindi  wa shindano la Mama shujaa wa Chakula 2015, Linaloendeshwa na Shirika la Oxfam kupitia program yake ya Grow msimu wa nne Caroline Chelele amekabidhiwa zawadi ya vifaa vya kilimo vyenye thamani ya kiasi cha shilingi Millioni 20, nyumbani kwake kata ya Ifakara mkoani Morogoro.
 
Akizungumza katika hafla ya makabidhiano hayo ya zawadi  Mkoani Morogoro wilayani Kilombero kata ya Ifakara,Meneja Ushawishi na Utetezi kutoka Shirika la Oxfam,Eluka Kibona alisema zawadi hiyo ni moja ya utekelezaji wa shindano hilo kwa mshindi aliyeshinda shindano hilo la Mama shujaa wa Chakula 2015.
 
Alisema shirika lao linatoa takribani Milioni 20 kwa mshindi ambapo mshindi  anatakiwakuchagua zawadi ya vifaa vya kilimo ili kuweza kumuwezesha zaidi. Kibona alisema Mshindi huyo alikabidhiwa Pawatila kwa ajili ya kubebea Mazao,vifaa vya umuagiliaji pamoja na Shamba lenye Ekali 7. 
 
“Huu ni muendelezo wa shindano la mama shujaa wa Chakula kukabidhi zawadi kwa ajili ya kuwainua wakulima wadogo wadogo kuonekana na Serikali kama wao wanamchango mkubwa kwa jamii
kutokana na Chakula wanacholima ndicho kinacholisha taifa,”alisema Kibona . Aliongeza shindano hilo lipo chini ya Kampeni ya GROW yenye lengo la kuwainua wakulima wadogo wanaokumbana na changamoto mbalimbali katika kilimo.
 
Kwa Upande wake Katibu Tawala wa Wilaya ya Kilombero , Yahya Naniya aliishukuru shirika hilo kwa hatua ya kuwathamini na kuwapigania wakulima wadogo ambao asilimia kubwa kati yao ni wanawake.Alisema
kupitia shindano hilo linaweza kuongeza Chachu kwa wakulima kufanya
shughuli za kilimo kwa kasi na kuongeza wigo mpana wa kupata mazao mengi kutokana na Mashirika mbalimbali kuwawezesha.
 

Naye Mshindi wa Shindano hilo 2015,Caroline Chelele alisema  atahakikisha zawadi hizo anazifanyia kazi ipasavyo itakayomuwezesha kumuongezea mazao mengi zaidi. Aliomba Serikali pamoja na mashirika mbalimbali kuendelea kuasidia wakulima wadogo na kuhakikisha nao
wanathaminiwa kama wakulima wakubwa.

No comments: