Thursday, November 26, 2015

NHC YAZINDUA MAUZO YA NYUMBA KATIKA MRADI WA KAWE JIJINI DAR ES SALAAM

NH9Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Bw. Nehemia Kyando Mchechu (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari Novemba 26, 2015 Jijini Dar es Salaam (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa mauzo ya nyumba katika mradi mpya wa Seven Eleven (711) ulioko Kawe Jijini Dar es Salaam (kulia) Mkurugenzi wa Usimamizi wa Miliki wa Shirika la Nyumba la Taifa, Hamad Abdallah.
NH2Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Bw. Nehemia Kyando Mchechu akiwaonesha waandishi wa habari michoro ya ramani ya mradi wa nyumba ulioko Kawe Jijini Dar es Salaam.
NH3Wafanyakazi wa NHC wakimsikiliza kwa umakini, Bw. Nehemia Kyando Mchechu.
NH4
NH1Mkutano ukiendelea.
NH5
Waandishi wa habari wakitembelea katika eneo la ujenzi huo.
NH6Ujenzi ukiendelea
NH7Ujenzi ukiendelea
NH8Waandshi wa habari pamoja na wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Bw. Nehemia Kyando Mchechu wakati wa uzinduzi huo.
Picha zote na Philemon Solomon-Fullshangweblog.
..................................................................................................
Na Philemon Solomon Fullshangweblog
SHIRIKA la Nyumba la Taifa (NHC) lazindua mauzo ya nyumba katika mradi wake mpya wa Seven Eleven (711) ulioko Kawe ,ambapo ujenzi huo ulianza Januari 2015.
Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi huo Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Bw. Nehemia Kyando Mchechu alisema ujenzi wa mradi huo unatarajiwa kukamilika ifikapo Desemba 2018 ,ikiwa ni takribani miezi 48 baada ya kuanza ujenzi. Mradi huo una ukubwa wa mita za mraba 111,842.90 ambao unatarajiwa kugarimu kiasi cha zaidi ya Sh 187, 927, 105,500 mpaka utakapomalizika .
Pia ikumbukwe kuwa mradi huu ni seemu ya mji mpya wa kisasa (Satellite City) unajengwa hapa ,mradi huu upo katika eneo tulivu la Kawe Jijini Dar es Salaam ambalo liko mita chache kutoka fuko za bahari ya Hindi pia karibu na maeneo muhimu kama Mbezi Beach, Masaki, Oysterbay, Morocco na Mikocheni mradi huu una jumla ya nyumba 422 za kuuzwa zilizopo kwenye majengo nane tofauti ya ghorofa 18 kila moja, ukiwa na huduma zote muhimu za kijamii.pia kutakuwepo na seemu ya maduka makubwa kwa ajili ya wakazi na maeneo ya jirani”Alisema Mchechu.

No comments: