Friday, August 28, 2015

MICHUANO YA WAVU YAANZA KURINDIMA ARUSHA

 Picha ikionyesha wachezaji wa timu ya pentagone ya jijini Arusha
Iliovaa bluu ikiwa inacheza na wachezaji wa timu ya Tanga katika
MICHUANO yamchezo wa wavu klabu Bingwa Taifa inaendelea kutimua vumbi jijini hapa ambapo timu ya mchezo wa wavu ya Tanga iliibuka kidedea kwa kuifunga timu ya pentagoni seti 3-1.
 wachezaji wa timu ya pentagoni wakiwa wanamsikiliza mwalimu.




picha zote na woinde shizza,Arusha

MICHUANO yamchezo wa wavu klabu bingwa taifa inaendelea kutimua vumbi jijini hapa hukuikizishuhudia timu shiriki zikichuana vikali kwa kuonyesha ubabe.

Katika ufunguzi  wa michuano hiyo timu za Pentagone na Flowers za
jijini Arusha zilifungua mashindano hayo ambapo zilifanikiwa kumaliza
 mchezo kwa timu ya Pentagone kuibuka na ushindi wa seti3-0 dhidi ya wapinzani wao.


Michezo mingine ilichezwa kwa wanaume ambapo ilizikutanisha timu ya  Dodoma ambayo iliibuka na ushindi wa  seti 3-0, dhidi ya Tanga, Karatu  walishinda seti 3-0 dhidi ya Flowers  hukukwa upande wa wanawake timu ya Dodoma ilichabangwa jumla ya seti 3-0 na wenzaoTanga. 

Mashindano hayo  yaliyoandaliwa na chama cha wavu
Tanzania(TAVA)  kwa Kushirikiana na chama chawavu mkoa Arusha
(AVA) yamekutanisha,mikoa mitatu pekee ambayo ni Arusha, Dodoma na Tanga
 huku vilabu sita kutoka mikoa hiyo ndivyo vinaonyeshana
ushindania mbavpo ni Pentagone klabu, Flowers Arusha, Karatu, JKT Mbweni ya Dar es salaam na Dodoma na Tanga vikiwakilishwa na timu mbili za wanaume na wanawake kilamoja.


Makamu Mwenyekiti wa chama cha wavu Tanzania (TAVA) Muharini Mchume alisema kuwa  mikoa mingine imeshindwa kushiriki kutokana na sababu mbalimbali za kwao kwani zilithibitisha kuja lakini hazikuweza kufika .

“Baadhi ya vilabu viliweza kutupa taarifa ya kushindwa kuja kwao katika mashindano hayo ikiwemo vilabu vya  jeshi na magereza ambavyo  vilitupa sababu yakuwa katika masuala ya ulinzi na usalama.
alifafanua Mchume.

Aidha alieleza zawadi mbalimbali zikiwemo medali na vikombe zawadi  hizo zitatolewa kwa washindi na kuongoza kuwa  Mabingwa watetezi wa michuano hiyo ya wavu mwaka 2014  timu ya Magereza kwa wanawake kutoka jijini Dar es salaam.

No comments: