Wednesday, July 29, 2015

WIZARA YA MAMBO YA NJE YAMUAGA BALOZI WA INDIA ALIYEMALIZA MUDA WA KAZI NCHINI


Balozi wa India nchini Tanzania anayemaliza muda wake wa kazi, Mhe.Debnath Shaw akitoa hotuba yake ya kuaga mbele ya wageni waalikwa wakiwemo  baadhi ya Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini wakiongozwa na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya wakati wa hafla ya chakula cha mchana iliyofanyika katika Hoteli ya New Afrika Jijini Dar es Salaam tarehe 29 Julai, 2015.

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya (kushoto) pamoja na Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo hapa nchini ambaye pia ni mkuu wa Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini, Mhe.Juma Halfan Mpango wakifuatilia hotuba ya Mhe.Debnath Shaw (hayupo pichani).
Balozi wa China hapa nchini, Mhe.LU Youqing (kulia) pamoja na Afisa  Mambo ya Nje, Bi.Eliet Magogo (katikati) pamoja na mmoja wa wageni waalikwa wakisikiliza hotuba.

Mabalozi pamoja na Maofisa wa Wizara ya Mambo ya Nje wakifurahia hotuba ya Balozi huyo wa India hapa nchini.
Balozi Yahya kwa pamoja na  Balozi Shaw wakitakiana afya njema
 Mshereheshaji akiendelea kusherehesha wakati wa hafla hiyo.
Balozi Yahya akiwaongoza Balozi  Shaw (kulia) na Balozi  Mpango kupata chakula wakati wa hafla fupi ya chakula cha mchan akumuaga Balozi Shaw.
 Balozi Yahya akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Shaw na Balozi Mpango
 Picha ya Pamoja.
 Balozi Simba akibadilishana mawazo na Balozi Debnath Shaw mara baada ya hafla hiyo.
Balozi Simba akiagana na Balozi Juma Mpango baada ya hafla hiyo Picha na Reuben Mchome

No comments: