Friday, July 31, 2015

KIDOTI :VIJANA WA JIJI LA ARUSHA CHANGAMKIENI FURSA ZA KIJASIRIAMALI



 Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Kidoti Jokate Mwegelo  (kidoti) akiwa na mabalozi wake aliwapata ndani ya mkoa wa Arusha tayari kwa kwenda mtaani kutangaza bidhaa zake zake za kidoti zilizoingia jijini Arusha kwa mara ya kwanza 



 warembo wa Kidoti wakiwa wako katika pozi wameshikilia baadhi ya bidhaa za Kidoti 


 mmoja wa mabalozi wa kidoti  aliyejulikana kwa jina la Anolia Agustino akiwa anaongea na waandishi wa habari


 Meneja masoko wa kampuni ya kidoti Peter Kasija akiwa anaongea na waandishi wa habari ndani ya viwanja vya triple A hii leo wakati walivyokuja jijini Arusha kutangaza bidhaa za kampuni yao
 mabalozi wa kidoti   wakiwa kazini
 baadhi ya bidhaa zinazosambazwa nakidoti jijini Arusha
 hizi ndizo ndala za kidoti
 mawigi ya kidoti ndio haya


Na Woinde Shizza 
wa libeneke la kaskazini blog

Wito umetolewa kwa vijana ndani ya jiji la Arusha kujitokeza katika
kuchangamkia fursa za kijasiriamali zinazojitokeza ili kuweza
kuwaepushia vijana na matendo maovu yanayoweza kuwafanya ndani ya
jamii kukosaa thamani.
Wito huo umetolewa na Joketi Mwigelwa (kidoti) wakati akichagua vijana
wajasiriamali ndani ya jiji la Arusha katika ukumbi wa triple A jijini
hapa ambapo anatarajia kuwapata wajasiriamali vijana ambao
hatawaingiza katika fursa ya wajasiriamali kwa kupitia kampuni yake ya
kidoti.

Alisema  kuwa amevutiwa  kuja kuwekeza ndani ya jiji la Arusha  katika
nyanza za ujasiriamali kwa kuwa anaelewa kuwa vijana wa jiji la Arusha
hususa ni wasichana wana muitikio mkubwa katika swala zima la
ujasiriamali na maendeleo binafsi.



Aidha alibainisha kuwa katika  mchakato huo wanatarajia kupata
wajasiriamali wapatao 13 ambapo tofauti na kujiingizia kipato cha
ujasiriamali pia watakuwa mabalozi wa kutangaza bidhaa zilizo chini ya
kampuni ya kidoti.
“ndugu mwandishi unavyowaona hawa wote hapa ni vijana kutoka mkoa
mzima wa arusha na mikoa ya jirani tunawafanyia usaili na kupata
vijana ambao wanakithi vigezo vya kuingia katika ujasiriamali ,utakao
wapelekea wao kufanya kazi na kampuni ya kidoti pamoja na kujiajiri
binafsi” alisema kidoti

Pamoja na hayo alisema kuwa kampuni hiyo kwa mwaka huu imeamua
makusudi kusogeza huduma za  ikiwemo bidhaa zake katika mikoa ya nje
ya jiji la Dar Es Salaam ili kuwapa furusa watu wa mikoani ambao
walikuwa hawazipati huduma za kidoti.

Kwa upande wa mmoja wa washiriki waliojitokeza katika mchujo huo
Anolia Agustino  alimpomgeza kidoti kwa hatuqa aliofikia ya kuwaajiri
vijana haswa wasiochana kwani   ,jambo hili litawasaidia wanasichana
wengi kupata ajira pamoja na kujiajiri binafsi.

Aidha alisema kuwa  mbali na kupata ajira pia kampuni hii itawasidia
kujifunza ujasiriamali pamoja na kujiajiri binafsi kwani ,bidhaa za
kidoti ni za bei na fuuu na unaweza kuanza kujiajiri kwa kutumia mtaji
mdogo.
Kwa upande wa mshiriki mungine ambaye teari alikuwa amenufaika na
kampuni ya kidoti aliyejitaja kwa jina la Anjela Mushi alisema kuwa
kampuni hii imemsaidia sana kwani alikuwa anakaa nyumbani bila kazi
lakini alivyoona kwenye mtandao wa kijamii aliamua kujitafuta
mawasiliano na kuanza  na mtaji mdogo na kwasasa ivi mtaji wake
umekuwa.

“mimi nilianza kuona bidhaa za kidoti katika mitandao ya kijamii kama
intagramu  nikaamua kutafuta mawasilano kwakeli nilipata na nilikuwa
na mtaji mdogo kwani nilianza na mtaji wa shilingi laki moja na sasa
na shilingi laki nne na biashara yangu nilianza mwezi wa tano na sasa
ni mwezi wa saba  kwa hadi sasa nina mienzi mitatu nashukuru mungu
mtaji wangu umekuwa”alisema Anjela.
Alimalizia kw akumpongeza kidoti na kumsihi aendelee kuwasaidia
wasichana kwani hivi sasa kumekuwa na changamoto ya ajira kwani ajira
imekuwa ni ngumu.

No comments: