Thursday, May 21, 2015

NMB Yafungua Tawi maalumu Oysterbay

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Saidi Meki Sadiki akiweka jiwe la msingi kwaajili ya uzinduzi rasmi wa tawi jipya na la kisasa la NMB Oysterplaza lililopo Oysterplaza jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa NMB – Tom Borghols huku meneja wa tawi hilo Donatus Richard akishuhudia. Tawi la NMB Oysterplaza ni maalumu kwa wateja wakubwa na wa kati.Kufunguliwa kwa tawi hilo kunafanya mkoa wa Dar es salaam kufikisha matawi 26 ya NMB.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Saidi Meki Sadiki akikata utepe kuashiria kuzinduliwa rasmi kwa tawi jipya na la kisasa la NMB Oysterplaza lililopo Oysterbay jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa NMB – Tom Borghols na kushoto ni Meneja wa tawi hilo - Donatus Richard na Meneja wa NMB Kanda ya Dar es Salaam – Salie Mlay. Tawi la NMB Oysterplaza ni maalumu kwa wateja wakubwa na wa kati. Kufunguliwa kwa tawi hilo kunafanya mkoa wa Dar es salaam kufikisha matawi 26 ya NMB.
Meneja NMB Kanda ya Dar es Salaam – Salie Mlay akiongea na wateja.
Kaimu Mkurugenzi wa NMB – Tom Borghols akiongea na wateja kabla ya uzinduzi wa tawi la NMB Oyster Plaza.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Dar es Salaam – Saidi Meki Sadiki akitoa hotuba ya ufunguzi wa tawi la NMB Oyster plaza.
Mgeni rasmi akiwa katika picha ya pamoja na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NMB – Tom Borghols, Mkuu wa kitengo cha wateja wadogo – Abdulmajid Nsekela, Meneja wa NMB kanda ya Dar es Salaam – Salie Mlay wakiwa kwenye picha ya pamoja na wafanyakazi wa NMB Oysterplaza.

No comments: