Monday, March 2, 2015

NHIF YAZINDUA HUDUMA ZA MATIBABU ZINAZOTOLEWA BURE NA MADAKTARI BINGWA-TABORA

Mkuu wa mkoa wa Tabora akihutubia wakati wa Uzinduzi wa huduma ya Madaktari bingwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Tabora Kitete,huduma ambayo inaratibiwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya NHIF ikiwa ni hatua ya kuwahamasisha wananchi kujiunga na Mfuko huo.
Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa  Bima ya Afya NHIF Bw.Charles Kajege akitoa maelezo kuhusu kuanzishwa kwa huduma hiyo ya Madaktari bingwa katika mikoa mbalimbali nchini ambayo imelenga kusaidia kutoa huduma za matibabu kwa watanzania kulingana na mahitaji ya maeneo husika. 
Mkuu wa mkoa wa Tabora  Bw.Ludovick Mwananzila akikabidhi msaada wa shuka kwa Mganga mkuu wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Tabora Kitete Dr.Gunini Kamba,katikati ni Katibu tawala mkoa wa Tabora Bi.Kudra Mwinyimvua.
Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya nchini NHIF Bw.Charles Kajege akikabidhi msaada wa vifaa tiba vitakavyosaidia zoezi la utoaji wa huduma za matibabu zitakazotolewa na madaktari bingwa kutoka hospitali ya Taifa ya Muhimbili na Taasisi ya Moi jijini Dar-es-Salaam.
Madaktari bingwa ambao watatoa huduma za matibabu bure kwa wananchi katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Tabora Kitete kwa muda wa siku saba.
Baadhi ya wananchi wakipanga hospitali ya rufaa Kitete wakisubiri kuonana na madaktari bingwa kwa ajili ya kupatiwa uchunguzi na matibabu.
Mganga mkuu wa mkoa wa Tabora Dr.Gunini Kamba akijaribu kuteta na viongozi wa ngazi ya juu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ambapo katikati ni Mjumbe wa bodi ya Wakurugenzi wa NHIF Bw.Charles Kajege,na kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya nchini Bw.Athuman Rehan.

No comments: