Wednesday, January 28, 2015

Ziara ya Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la Nyumba la Taifa NHC mikoani

New Picture (4) 
Ujumbe wa Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu wakikagua eneo lililotengwa kwa ajili ya NHC kujenga nyumba za gharama nafuukatika Halmashauri ya Wilaya Serengeti-Mugumu. Eneo hili lina ekari 134 na miundombinu ya maji na umeme.
New Picture (5) 
Afisa Mipango Miji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mugumu Serengeti akimuonyesha Mkurugenzi Mkuu wa NHC ramani ya mpango Miji inayoonyesha eneo la NHC la kujenga nyumba za gharama nafuu.
New Picture (6)Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu akiongea na kikundi cha vijana Wilayani Serengeti waliyosaidiwa mashine na NHC kwa ajili ya kujiajiri kupitia utengenezaji wa matofali yanayofungamana
New Picture (7)Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu na ujumbe wake wakikagua jingo la biashara lililojengwa na NHC eneo la Mukendo Musoma.

New Picture (8)Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu akitoa maelekezo ya matumizi bora ya dari la jengo la biashara la Mukendo lililojengwa na NHC katika Manispaa ya Musoma ili kuongeza mapato ya Shirika.
New Picture (9)Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu akikagua ujenzi wa nyumba za gharama nafuu zinazojengwa na NHC eneo la Buhare Musoma. Jumla ya nyumba 50 zinatarajiwa kukamilika Julai 2015.
New Picture (10)Vijana wakishiriki kujenga misingi ya nyumba za gharama nafuu eneo la Buhare Manispaa ya Musoma
New Picture (11)Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu akijadili namna ya kuongeza ubora wa nyumba za gharama nafuu zinazojengwa na NHC katika maeneo mbalimbali nchini. Amesisitiza kupunguza gharama ya ujenzi ili nyumba zinazojengwa ziwe nafuu.
New Picture (12)Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu na ujumbe wake walipotembelea Wilayani Tarime kujionea nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na NHC mwaka 1968 na ambazo hadi hivi sasa zinasaidia familia mbalimbali. Nyumba hizi ni za vyumba viwili na zilipewa Halmashauri hiyo mwaka 1991.
New Picture (13)Ujumbe wa Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu ukiwa eneo la Isibania nchini Kenya kujionea namna nchi hiyo ilivyopanga eneo lao la mpakani.
New Picture (14)Ujumbe wa Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu ukiwa eneo la Sirari kuona eneo la kujenga nyumba ili kuboresha taswira ya mpaka wa nchi yetu. Ujumbuliongozwa na Maafisa Ardhi wa Wilaya ya Tarime.
New Picture (15)Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu na ujumbe wake pamoja naongozi wa Wilaya ya Butiama wakikagua eneo lililotengwa na Wilaya hiyo ili NHC ijenge nyumba za gharama nafuu. Bw. Mchechu amesisitiza kuwa NHC itajenga nyumba katika Wilaya hiyo ili kuenzi mchango wa Mwalimu Nyerere wa kulianzisha Shirika la Nyumba la kwanza nchini Tanzania mwaka mmoja tu baada ya uhuru.
New Picture (17)Ujumbe wa Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu ukiangalia mnara wa kumbukumbu ya mahali ambapo ilikuwepo nyumba aliyozaliwa Baba wa Taifa.
New Picture (18)
New Picture (19)Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu aliwa amekaa sehemu maarufu aliyokuwa akikaa Mwalimu Nyerere wakati wa kucheza bao.
New Picture (20)Hapa ndipo alipozikwa Hayati Mwalimu Nyerere. Ujumbe wa NHC ulizuru makumbusho ya Mwalimu kama sehemu ya kuenzi mchango wake wa kulianzisha Shirika la Nyumba mwaka mmoja tu baada ya uhuru wa Tanganyika.
New Picture (22)Picha ya pamoja ya Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu na kikundi cha vijana cha Samaritans Association cha Wilaya ya Bunda kilichofadhiliwa na NHC mashine za kutengeneza matofali New Picture (23)Bw. Yoramu Salum ambaye ni Afisa Mipango Miji katika Halmashauri ya Busega akionyesha ujumbe wa NHC eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa nyumba.
New Picture (24)Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu akiwa katika picha ya pamoja na mojawapo ya kikundi cha vijana kilichofadhiliwa na NHC mashine za kufyatua tofali ili kukuza ajira Wilayani Magu
New Picture (25)Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu akipokea risala aliyosomewa na kikundi cha vijana Wilayani Magu. Anayekabidhi vijana hao fedha zilizotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa NHC ni Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya hiyo Mwalimu Naomi Nnko.
New Picture (26)Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Magu Bibi Naomi Nnko wakikagua ramani inayoonyesha viwanja vya NHC vya kujenga nyumba za gharama nafuu.

No comments: