Saturday, December 13, 2014

Hafla ya kukabidhi Mgodi wa Resolute kwa Chuo cha Madini Dodoma

 Naibu Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia Madini, Mhe Stephen Masele (aliyesimama katikati na pama) akishuhudia halfa fupi ya kusaini makabidhiano ya eneo la Mgodi wa Resolute kwa Chuo cha Madini Dodoma. Wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Chuo cha  Madini Dodoma, Mjiolojia Mwandamizi Subian Chiragwile, katikati ni Kaimu Kamishna wa Madini Mhandisi Ally Samaje, na kushoto ni Meneja Mkuu wa Mgodi wa Resolute Peter Beilby. Wengine wanaoshuhudia ni Mkuu wa Wilaya ya Nzega Bintuni Msangi (wa pili kuchoto aliyesimama),Mkurugenzi Kampuni ya Resolute Rose Aziz na baadhi ya waliohudhuria.
 Meneja Mazingira   baada Mgodi wa Resolute Jackie Sinclair (Kulia), akimkabidhi funguo mbalimbali za majengo ya eneo la mgodi wa Resolute Naibu Waziri wa Nishati na Madini (Madini)  Stephen Masele (Kushoto) mara  makabidhiano ya eneo la mgodi.
 Naibu Waziri wa Nishati na Madini Stephen Masele (kushoto) akimkabidhi Mkuu wa Chuo cha Madini Dodoma Mjiolojia Mwandamizi Subian Chirangilwe funguo mbalimbali za majengo ya mgodi wa Resolute kwa ajili ya Chuo cha Madini Dodoma.
 Meneja Mkuu wa Mgodi wa Resolute Perer Beilby   (wa pili kulia) akimwogongoza Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Stephen Masele kukagua maeneo mbalimbali ya Mgodi wa Resolute ambao yamekabidhiwa kwa Chuo cha Madini Dodoma.
 Naibu Waziri wa Nishati na Madini Stephen Masele akiangalia chumba cha Computer ambacho ni miongoni mwa vifaa ambavyo Mgodi wa Resolute umekabidhi kwa ajili ya Chuo cha Madini Dodoma.
 Meneja Mazingira wa mgodi wa Resolute Jackie Sinclair (mbelea) akieleza jambo wakati akikiabidhi baadhi ya vifaa vya maabara kwa Chuo cha Madini Dodoma. Wanaomsikiliza ni Naibu Waziri wa Nishati na Madini Stephen Masele  ujumbe alioambatana nao.
 Meneja Mazingira wa Mgodi wa Resolute Jackie Sinclair akikabidhi  moja ya vifaa ambavyo vitatumiwa na Chuo cha Madini Dodoma kwa wanafunzi kujifunza kwa vitendo wakati wa halfa ya kukabidhiana eneo la mgodi wa Resolute. Wanaoangalia kutoka kushoto ni Naibu Waziri  wa Nishati na Madini Stephen Masele, Kaimu Kamishna wa Madini Mhandisi Ally Samaje na Mkuu wa Wilaya ya Nzega Bintuni Msangi
 Sehemu  mgodi ambao shughuli za uchimbaji zilikuwa zikifanywa na mgodi wa Resolute ambao pia umekabidhiwa kwa Chuo cha Madini Dodoma. Kwa mujibu wa Mkuu wa Chuo Madini Dodoma Mjiolojia Mwandamizi Subian Chirangilwe ameeleza kuwa,mgodi huo utatoa fursa kwa wanafunzi kujifunza kwa vitendo kuhusu shughuli za uchumbaji.
Baadhi ya wageni waliohudhuria hafla ya makabidhiano ya eneeo la Mgodi kwa Chuo cha Madini Dodoma wakifuatilia hotuba ya makabidhiano ya mgodi huo.

No comments: