Sunday, September 21, 2014

Simba yatoka sare ya 2-2 na Coast union Uwanja wa Taifa jijini Dar leo

Beki wa Simba, Mohamed Hussein (kulia) akichuana na Seleman Rajab. Timu hizo zilitoka sare ya 2-2.
Emmanuel Okwi akiwania mpira na beki wa Coast Union.
 Umati wa mashabiki waliofika uwanja wa Taifa.
 Mshambuliaji wa Simba, Ramadhan Singano 'Messi' akimiliki mpira huku akizongwa na beki wa Coast Union, Abdallah Mfuko.
Mshambuliaji wa Simba, Haruna Chanongo akiruka daruga la beki wa Coast Union. 
 Hamis Tambwe akitafuta mbinu za kumtoka beki wa Coast Union.
Hatari katika lango la Coast Union.
Emmanuel Okwi akimtoka beki wa Coast Union.
 Kikosi cha Simba.
 Kikosi cha Coast Union.
 Golikipa wa Coast Union ya Tanga, Shaban Kado akiokoa moja ya hatari langoni mwake.

Wachezaji wa Coast Union wakitoka mapumziko.

Wachezaji wa Simba wakitoka mapumziko.
 Benchi la ufundi la Coast Union.
 Manahodha wa Simba na Coast Union wakiwa katika picha ya pamoja.
Benchi la ufundi la Simba likiongozwa na Patrick Phil.
Kikundi cha New Mapambano kikitumbuiza wakati Simba ikipambana na Coast Union.
 Mashabiki wa Simba wakiwa na uzi wa Simba.
 Mashabiki wa Simba wakiishangilia timu yao.
 Wachezaji wa Simba wakishangilia bao la kwanza la timu hiyo kabla Coast Union kusawazisha.
Mshambuliaji wa Simba, Amis Tambwe akiifungia timu yake bao la pili wakati timu hiyo ilipopambana na Coast Union ya Tanga katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Timu hizo zilitoka sare ya 2-2.

No comments: