Wednesday, August 20, 2014

Redds Miss Temeke 2014 kujulikana ijumaa TCC Club,Chang'ombe,jijini Dar

 Warembo watakaoshiriki mashindano ya Redd's  Miss Temeke, wakiwa katika picha ya pamoja na Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Khalid Mohamed (TID), anayemiliki bendi ya  Top in Town,itakayotoa burudani katika mashindano hayo.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Khalid Mohamed (TID), anayemiliki bendi ya  Top in Town, akielezea katika mkutano na waandishi wa habari, katika  klabu ya City Sports & Lounge jinsi alivyojiandaa kutoa burudani katika mashindano ya Redd's Miss Temeke yatakayofanyika ijumaa ndani ya TCC Club,Chang'ombe, Dar es Salaam. Kulia kwake ni Mwandaaji wa mashindano hayo, Benny Kisaka.Nyuma yao ni baadhi ya warembo watakaoshiriki mashindano hayo. 

MALKIA wa kanda ya Temeke, Redds Miss  Temeke 2014 anatarajiwa kupatikana Ijumaa   Agosti 22, mwaka huu kwenye ukumbi wa TCC  Club Chang'ombe.Jumla ya warembo 17 kutoka vitongoji vya Mbagala, Kurasini na Chang;ombe watapanda  jukwaani jukwaani kuwania taji hilo.



Alisema kuwa mbali ya shindano hilo kubwa, kulifanyika shindano dogo la awali  lililoandaliwa na Michuzi Media Group la Miss  Photogenic ambalo mshindi wake atazawadiwa  kitita cha Sh. milioni 1 taslimu, shindano ambalo lililsimamiwa na jopo la wapiga picha wa kampuni hiyo ambao watamtangaza na  kumpa zawadi mshindi siku ya shindano.



Alisema mkali wa bongofleva, Khalid Mohamed  TID almaarufu kama Top in Dar, sanjari na  Wanne Star, Makirikiri wa Tanzania, Young  Suma, Super Bokilo na wasanii mbalimbali  wanatarajia kupamba shoo hiyo ambayo Dj John  Peter Pantelakis atalisindikiza. 


Wadhamini wa shindano hilo ni TBL Kupitia  Redds wamedhamini shindano hilo sanjari na kinywaji cha Zanzi, Michuzi Media Group, Radio  EFM 93.7 Cash & Carry Distributors, Kitwe General Traders, Rio Gym & Spa, CXC Africa, 88. 5 Clouds FM, City Sports Lounge, Gazeti la  Jambo Leo, Kiwango Security na 100.5 Times FM.

BMP Promotions imeshakamilisha shindano hili  la 19 tangu kuanzishwa Miss Temeke chini ya undaaji wake kwa asilimia kubwa, hivyo  washabiki wa Kanda ya Temeke na vitongoji  vyake watarajie mabadiliko makubwa katika aina  ya shindano la urembo litakavyokuwa Ijumaa. 

1996- Asela Magaka 1997- Miriam Odemba 1998- Khamisa Ahmed (Miss Temeke  anayeendea kujiita hivyo huko Marekani) 1999- Ediltruda Kalikawe 2000- Irene Kiwia 2001- Happyness Sosthnes Magesse super model  Millen( Miss Tanzania) 2002- Regina Mosha 2003- Hawa Ismail ( Sylvia Bahame first runner  up and Miss Tanzania same year) 2004- Cecylia Assey ( mrs Agrey Marealle), first  runner up Miss Tanzania


2005- Seba Aggrey 2006- Jokate Mwegelo (Miss Tanzania fisrt  runner up), Irene Uwoya 1st  runner Temeke &  3rd runner up Miss Tanzania

2007- Queen David ( Miss Tanzania second runner up)
2008- Angela Lubala (top five Miss Tanzania) 
2009- Sia Ndaskoy (top five Miss Tanzania)
2010- Genevieve Mpangala ( Miss Tanzania)
2011- Husna Twalib
2012- Edda Sylvester





runner up  Miss Tanzania)

No comments: